• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

BARAZA LA MADIWANI KUPITISHA TAARIFA ZA ROBO YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: February 10th, 2023

Baraza la Madiwani Wilaya ya Kibiti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 limekutana katika ukumbi wa Halmashauri kujadili taarifa mbalimbali za robo ya pili  na wote kwa pamoja wameridhia na kuzipitisha.

Awali Mkurugenzi Mtendaji Mohamed Mavura ambaye alikuwa Katibu wa baraza hilo akitoa taarifa ya wilaya amesema kumekuwa na wimbi la uuzaji holela wa ardhi hivyo ameandika barua ya zuio la uuzaji wa maeneo hovyo na amewaagiza  watendaji wote kusimamia kikamilifu jambo hilo. Kwa upande wamaafa ya hivi karibuni yaliyotokana upepo mkali  na mvua zinazoendelea kunyesha amewataka Madiwani kushirikiana na viongozi wa vijiji au kata Pamoja na wananchi kutatua changamoto ndogodogo ambazo zipo ndani ya uwezo wao kuliko kuendelea kusubiri Halmashauri ifanye Kila kitu.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kibiti Mhe. Ramadhan Mpendu akimkaribisha Mkuu wa Wilaya  ambaye anashiriki kwa mara ya kwanza katika baraza la madiwani Wilayani Kibiti, amempongeza Mkuu wa wilaya ya Kibiti Kanali Kolombo kwa kuteuliwa na Rais na kuahidi kumpa ushirikiano wa kutosha katika utendaji. Vilevile amepongeza mkuu wa wilaya ya Rufiji aliyekuwa akikaimu kwa muda wa miezi kadhaa kwa kazi nzuri aliyoifanya Wilaya ya Kibiti licha ya kuwa na majukumu mengi.

Katika baraza hilo Mpendu amewasihi viongozi kumuunga mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha watoto wote wanakwenda shule katika ngazi ya msingi na sekondari kwani elimu ni bure na amefanya jitihada nyingi kupunguza kero kwa kujenga shule nyingi karibu na jamii jambo linalowapunguzia safari watoto kutembea mwendo mrefu kwenda shule.

Vilevile Mpendu amesisitiza wananchi wa kibiti kutumia vizuri msimu huu wa mvua kwa kulima mazao ya biashara na chakula wa wingi ili kuweza kuwa na uhakika wa kuwa chakula cha kutosha na  siyo kulima mazao ya biashara pekee.

Akitoa salamu za serikali Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali  Joseph Kolombo amelishukuru baraza la Madiwani kwa mshikikamano na kuwataka kuendelea kudumisha ushirikiano kuhakikisha kibiti inasonga mbele.

Kanali kolombo amewataka  madiwani na watendaji wote kuhakikisha wanasimamia vizuri miradi ya maendeleo ili mwenge wa uhuru utakapokaguwa miradi ya maendeleo mwaka huu kusiwe na dosari ya aina yeyote.

“tujiandae mwenge utakagua miradi ya maendeleo tusimamie vizuri ukaguzi usiwe na dosari” Alisema Kanali Kolombo.

Pia Mkuu wa wilaya Kolombo ameagiza watendaji na Madiwani kutambua idadi ya wanyama waliopo kwa makundi ili kuruhusu zoezi la kuanza kugawa maeneo ya vitalu vya kufugia (Ranchi ndogo ndogo) kwa ajili ya wafugaji kuweza kufugia mifugo yao kama serikali ilivyoagiza.

Aidha amewataka Wazazi wa kata ya msala kupeleka watoto katika shule ya nyamisati inayotoa huduma kwa sasa wakati wakisubiri kukamilika kwa ujenzi wa shule mpya katika maeneo na siyo kukaa na watoto majumbani.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya kibiti Juma Ndaruke katika baraza hilo amelitaka shirika la umeme TANESCO kuhakikisha linapata muafaka juu ya tatizo la kukatika Kwa umeme mara kwa mara Pamoja na kuimarisha njia za mapitio ya umeme  ikiwa ni pamoja na kukata miti iliyokaribu nan jia za  umeme.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.