• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

BEI YA MBAAZI KWA KILO YAWAPA MATUMAINI WAKULIMA WA ZAO HILO.

Posted on: September 14th, 2024

Wakulima wa mbaazi Mkoa wa Pwani wameonekana kufurahishwa na kupata matumaini ya bei ya zao hilo ambalo kimauzo lilikuwa chini zaidi  ukilinganisha na mazao ya Korosho na Ufuta.

Hayo yamejiri katika Mnada wa pili wa zao la mbaazi Mkoa wa Pwani ambao umefanyika tarehe 13.09.2024 Wilayani Kibiti. Katika mnada huo Kibiti imefanikiwa kuuza jumla ya Tani 19 na kg 667 kati ya Tani 122 na kg769 zilizouzwa kwa Mkoa mzima baada ya wakulima wote kuridhia kwa pamoja.

Baada ya kuchakata bei katika mnada huo, mbaazi zimeuzwa kwa bei ya wastani ya sh 1753.88 kwa kilo ambapo bei ya juu ilikuwa Sh.1760 na bei ya chini Sh.1750.


Mara baada ya mnada huo kumalizika Meneja wa CORECU Mkoa wa Pwani Ndg. Hamis Mantawela ametoa rai kwa wakulima wa mbaazi Mkoani humo kulichukulia zao hilo mbadala la kibiashara kuwa fursa kwa kuhakikisha wanakuwa na  mbaazi bora zilizokauka vizuri.

Vilevile Bw. Mantawela amewataka wakulima ambao bado wanavuna kuongeza kasi zaidi  na kufikisha mapema mazao yao ghalani hususani wakati huu ambao bei bado ni nzuri.


Aidha Mwakilishi wa wakulima wa mbaazi Ndg.Kassim Juma  amesema kwa mwenendo wanaouona wa bei ya mbaazi kwa kilo wamefarijika na kufurahishwa sana kwani mnada umeleta matumaini, walizoea kuuza zao hilo kwa  bei ya chini ambapo kwa wastani walikuwa wakiuza Sh. 200-300 kwa kilo.


Hata hivyo Ndg. Kassim amesema anatumaini mnada ujao wakulima wataongezeka kwa kasi zaidi lakini pia amewataka wakulima wenzake kuandaa mbegu bora mapema kwa ajili ya msimu ujao huku akisisitiza kutenga maeneo kwa ajili ya kilimo hicho.


"Wakulima wenzangu hii ni fursa, kama kuna mkulima analima ekari 20 za ufuta au korosho, basi atenge angalau eka 4 kwa ajili ya Kilimo cha mbaazi" Alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.