• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DC KOLOMBO ATEMBELEA MIRADI KIBITI

Posted on: February 9th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amefanya ziara ya kikazi kukagua eneo la ujenzi wa chuo cha ufundi (VETA) katika kijiji cha Nyambili  unaotarajiwa kuanza hivi karibuni ikiwa ni sehemu ya kuongeza wingo wa kitaaluma katika ngazi ya wilaya kwa watoto ambao hawakupata nafasi ya kwenda elimu juu kujiendeleza.

Awali Mtendaji wa Kijiji cha Nyambili Elia Clemence akimkaribisha mkuu wa Wilaya amesema eneo hilo lilitengwa na Serikali ya Kijiji ni salama, lina jumla ya hekta 267ambapo kati ya hizo heka 50 zimetengwa  maalum kwa ajili ya ujenzi wa chou hicho.

 Kanali Kolombo amesema lengo la ziara yake ni kufika na kujiridhisha  juu ya uwepo wa eneo hilo

Aidha, Kanali Kolombo ameagiza Kijiji kuandika muhtasari utakaoainisha maeneo yaliyowazi ili kutambua akiba iliyopo kwa ajili ya shughuli nyingine za maendeleo. Sambamba na hayo amewaagiza Wataalam wa ardhi kupima eneo na kuhakikisha upatikanaji wa Hati Pia amewataka wakuu wa Taasisi za TARURA,TANESCO na Idara ya maji kupima na kuweka miundombinu muhimu ikiwa ni pamoja na barabara, umeme na maji.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya Mhe. Kolombo ametembelea shule mpya ya sekondari Nyambili Nyambunda na kuagiza kuendeleza zoezi la kutoa elimu kwa jamii kuona umuhimu wa watoto kuripoti shule na kuchangia Jumla ya sh 130,000 kwa ajili ya chakula shuleni.

Wakiwa shuleni hapo, Mohamed Mavura ametoa rai kwa wazazi na jamii kwa ujumla katika msimu huu wa kilimo kuhakikisha wanalima mazao ya vyakula jambo litakalorahisisha uchangiaji wa chakula shuleni bila kutumia  gharama kubwa.

Kwa mujibu wa Mwalimu wa chakula shuleni hapo amesema katika shule hiyo wameshaanza kulima mbogamboga, migomba, mihogo sambamba na zoezi la kupanda miti ambapo mpaka sasa jumla ya miti 700 kati ya 1400 imeshapandwa.

Vile vile, Kanali Kolombo amekagua kituo cha Polisi Jaribu mpakani ambacho kipo katika hatua ya umaliziaji na kituo cha Polisi bungu ambacho kipo katika hatua ya upandishaji ukuta na kuchangia sh 200,000 Kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huo na kusisitiza ujenzi huo kukamilika kwa wakati.

Hata hiyo Mhe. Kolombo amekagua ujenzi wa barabara ya mzunguko ya stendi ya wilaya ya Kibiti inayojengwa kwa kiwango cha lami na kumtaka mkandarasi kuripoti ofisini kwake katika siku ya ijumaa(kesho) tar 10/02/2023 ili kuweka makubaliano ya ni lini ujenzi unakamilika ukizingatia mkataba wake upo ukingoni kumalizika na kazi bado haijaisha.

.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.