• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DC KOLOMBO ATIMIZA AHADI KIJIJI CHA NYANJATI, AKABIDHI MABATI 120 KATI YA 148.

Posted on: February 11th, 2024

February 5, 2024 Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amekabidhi mabati 120 kwa ajili ya kuezeka boma la nyumba ya mwalimu katika Kijiji cha Nyanjati Kata ya Mahege,  ikiwa ni sehemu ya kutimiza ahadi yake ya kuwapatia mabati 80 aliyoitoa tarehe 29/01/2024.

"Leo nimetimiza ahadi yangu,Serikali yenu iko makini, ni sikivu na inawajali, na leo tunakabidhi mabati 120 na siyo 80 tena  kama nilivyoahidi Awali, sasa kazi iendelee" Alisema Kanali Kolombo.

Mara baada ya kukabidhi mabati hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kibiti Ndg. Hemed Magaro alisema kuwa, kabla ya kuleta mabati hayo walifanya upembuzi yakinifu  na Mhandisi wa majengo na kubaini jumla ya mabati yanayotakiwa ni 148.

"Tulifanya tathmini na kubaini boma linahitaji mabati 148, tumekabidi 120 hivyo bado tuna upungufu wa mabati 28 na yatakuja". Alisema Magaro.


Vilevile Mkurugenzi Magaro amesema kwa upande wa boma la nyumba ya Mganga (Afya) tayari  limekwishaingizwa kwenye mpango  na jengo la utawala litasubiri bajeti ijayo na litakamilika kwa kadri bajeti itakavyoruhusu.

Aidha Mkuu wa Taasisi ya kupambana na rushwa Wilaya ya Kibiti Bi Anna Shine amewataka wakazi wa Kijiji cha Nyanjati kuhakikisha mabati waliyokabidhiwa yanafanya kazi iliyokusudiwa na si vinginevyo. 

"Hiyo ni fedha ya Serikali, mkayatumie mabati haya kama inavyotakiwa" Alisema Bi Anna kwa msisitizo.

Mwisho Viongozi wa Kata hiyo wamewashukuru viongozi wote wa Halmashauri, kwa kufanya kazi kwa vitendo na kudai kwamba upokeji wa mabati hayo utawafanya watembee kifua mbele kwa wananchi wakiwa na neno la kusema na sasa hata wakiitisha vikao ,wananchi wataitikia wito.

Awali wajumbe  (Viongozi) hao waligoma kuendelea kushiriki vikao vya aina yeyote kijijini hapo mpaka wajue hatma ya ukamilishaji wa maboma hayo kwani yalifanya waonekane wababaishaji kwenye jamii.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.