• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DC KOLOMBO ATOA WIKI 2 KUTATUA KERO ZA MAJI KIBITI.

Posted on: June 26th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo ametoa wiki 2 kwa RUWASA Wilaya ya Kibiti kuhakikisha wanatatua kero za wananchi zinazohusiana na maji.

"Ninawapa wiki mbili kuhakikisha kero za Wananchi zinazohusiana na maji mmezipatia ufumbuzi, watu wanahitaji maji na sio maneno, nendeni mkawasililize msikae ofisini" Alisema.

Hayo yamejiri katika Mkutano Mkuu wa pili wa wadau wa sekta ya maji vijijini na wakala wa Maji na usafi wa Mazingira vijijini uliofanyika tarehe 24.06.2024 katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya wavulana Kibiti.

Akifungua mkutano huo Kanali Kolombo alimpongeza Mhe. Rais Dkt. SSH kwa kutoa fedha za miradi ya maji kibiti. Pia alieleza kuwa lengo la mkutano huo ni kutathmini hali ya maji, kuweza kutambua changamoto zolizopo na kuboresha mapungufu ili miradi hiyo iweze kuwa endelevu kwa kutoa maji muda mrefu.

Hata hivyo mewaagiza Viongozi kuhakikisha wanasimamia vizuri miradi ya maji ikiwa ni pamoja na kuimarisha ulinzi wa miundombinu hiyo huku akiwashukuru wajumbe na wadau hao wa maji kwa kushiriki mkutano huo.

Mkutano huo ulioongozwa na Mkuu wa wilaya ulishirikisha wadau mbalimbali wa maji wakiwemo Madiwani, watendaji wa Kata, watendaji wa vijiji, wenyeviti wa vijiji na Vitongoji ambao pia waliweza kuelezea kero za wananchi kuhusu maji.

Katika mkutano huo Makamu Mwenyekiti wa baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti  Mhe. Omari Twanga amewataka RUWASA na watendaji wengine wa Serikali kuendelea kushirikiana kwa dhati kwa kuibua changamoto zilizopo na kuzipatia suluhisho ili kuweza kutimiza lengo la Serikali ya kila mwananchi kupata maji safi na salama katika maeneo ya karibu.

Aidha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Denis Kitali aliwataka RUWASA kukabiliana na changamoto zolizopo kwa kuzipatia ufumbuzi kwani suala la maji linamgusa kila mtu na kazi kubwa ya Serikali ni kutekeleza ilani iliyopo madarakani kwa kuwahudumia wananchi.

Naye Kaimu Meneja wa RUWASA Kibiti Mhandisi Juma Ndaro Alisema ngazi ya Wilaya wameweka mikakati kabambe ikiwa ni pamoja na mpango wa kuhakikisha wanafikia 85% usambazaji wa maji kwa kuibua miradi mipya ya maji na kukarabati ya zamani.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.