• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DC KOLOMBO: WAPELEKENI WATOTO WAKAPATE CHANJO YA SURUA NA RUBELLA (TAREHE 15-18 FEBRUARI 2024)

Posted on: February 14th, 2024

NI KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA AFYA MSINGI.

Katika kuhakikisha chanjo mbalimbali zinawafikia wananchi nchini  Wizara ya Afya Ofisi ya Rais Tamisemi imeandaa kampeni ya kitaifa ya kutoa chanjo ya Surua na Rubella kwa watoto wote walio na umri wa miezi 9 mpaka chini ya miaka 5 kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo. Kampeni hii itaanza tarehe 15/02/2024 hadi 18/02/2024.


"Lengo la kampeni hii ni kuongeza Kinga kwa walengwa kwa kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa Surua na Rubella kwa watoto wote bila kujali kuna aliyekwishapata chanjo Awali au la" Alisema Frank Patrick Mratibu wa chanjo Wilaya ya Kibiti.

Katika kikao hicho Mratibu huyo amesema mkakati wa utoaji wa chanjo utahusisha vituo vya kudumu vya kutolea huduma za Afya, huduma za mkoba na kliniki tembezi kwa vituo na vituo vya kuhamahama vitakavyopangwa. Vilevile  amesema utoaji wa chanjo hizo utatekelezwa katika maeneo mbalimbali kama vile sokoni, shuleni, nyumba za Ibada, vituo vya mabasi, kambi za wavuvi, wakimbizi ,vituo vya mipakani na popote penye watoto.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya Daktari Elizabeth Oming'o amesema ni muhimu kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo hususani watoto wa kike kwani madhara ya magonjwa hayo ni makubwa yakipuuzwa ikiwa ni pamoja hapo baadaye kuzaa mtoto aliyefia tumboni, kiziwi, mlemavu, kuzaa mtoto mwenye moyo wenye tundu na hata kusababisha vifo kwa sababu mara nyingi huambatana na homa Kali.

Akizindua kampeni hiyo Mkuu wa wilaya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema utoaji wa chanjo utasaidia kuzuia kuenea kwa magonjwa hayo. Hivyo amewataka wazazi na walezi wote wenye watoto wenye umri uliotajwa kuhakikisha wanawapeleka watoto wao kupata chanjo.

Mara baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo, Kanali Kolombo ameiagiza Idara ya Afya kutoa matangazo na  kutengeneza vipeperushi vinavyoeleza umuhimu wa chanjo hiyo haraka na Vituo vitakavyohusishwa na kuvisambaza sehemu mbalimbali ili jamii ipate kutambua ni zoezi linaloendekea nchini.

"Zoezi hili linafanyika nchi nzima, sambazeni taarifa haraka ili kurahisisha kampeni hii kufanyika kwa wakati uliopangwa" Alisema Kanali Kolombo.

Mbali na agizo hilo amewataka wananchi wote kuwa mabalozi wa chanjo kwa kuhakikisha kila anayepata ama kusikia tangazo hilo linalohusu Chanjo basi anamjulisha mwenzake kupeleka mtoto wake kwenda kupata chanjo kwani Surua na Rubella ni magonjwa yanayoweza kukingwa kwa njia ya chanjo hivyo yasipuuzwe.

Aidha ametoa  angalizo la ujumbe muhimu kwa wananchi kuhakikisha wanatoa taarifa haraka juu ya madhara atakayopata mtoto baada ya kupewa chanjo au  kuona mgonjwa mwenye  dalili za homa na vipele kooni na mwilini.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.