• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DED MAGARO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KIBITI

Posted on: April 5th, 2024

3.4.2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg Hemed Magaro na Wataalam wake wamefanya ziara ya kawaida kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo katika Kata ya Dimani na Kibiti.

Kati ya miradi iliyokaguliwa ni pamoja na Ujenzi  wa chumba kimoja cha darasa shule ya Sekondari Dimani chenye thamani ya sh. 26,000,000 ambacho kimekamilika pamoja na choo chenye thamani ya sh 4,000,000 ambacho Ujenzi wake upo katika hatua ya kupandishwa ukuta huku shimo la choo hicho likiwa limeshachimbwa na ujenzi ukitarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa.

Vilevile wamekagua Ujenzi wa matundu matano ya choo pamoja  na shimo la maji taka vyenye thamani ya sh 6,600,000 katika shule ya Msingi kimbuga. Ujenzi wa choo hicho upo katika hatua ya linter.

Hawakuishia hapo pia wamekagua Ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na viwili vya Ofisi katika shule ya Sekondari ya Wananchi ambavyo mpaka sasa vimefikia usawa wa linter ujenzi huo ni nguvu za wananchi. Pia Halmashauri imepokea Tsh. Milioni mia nne (400,000,000/=) ambapo Milioni 50 ni za umaliziaji wa vyumba vinne vya madarasa na Ofisi mbili, na Milioni 350 ni za ujenzi wa madarasa, jengo la utawala, vyoo, maabara tatu pamoja na mfumo wa maji.

Mbali na kazi hizo pia wamekagua Ujenzi wa choo cha matundu manne katika shule ya Msingi Nyamakonge wenye thamani ya sh 7,200,000 chini ya mradi wa EP4R ambao umekamilika licha ya kuwepo kwa kasoro ndogo ndogo.

Hata hivyo wamekagua Ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi ambao upo katika hatua ya umaliziaji sambamba na ukaguzi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya Wilaya ambapo Ujenzi unaendelea.

Mara baada ya kukagua na kujionea hali halisi, Mkurugenzi Magaro amewaagiza Muhandisi (W), Wasimamizi wa ujenzi na Mafundi kuhakikisha wanakamilisha majenzi yote kwa wakati uliokusudiwa hususani katika Sekondari ya Dimani, kufanya tathmini ya gharama za kumalizia Ujenzi wa choo shule ya Msingi kimbuga na kuziwasilisha wilayani. 

Pia katika shule ya Sekondari ya Wananchi amekagua maandalizi ya ujenzi na kuagiza ujenzi huo kuanza mara moja kwani fedha zipo tayari, na kwa Shule ya Msingi Nyamakonge ameelekeza kuhakikisha wanarekebisha kasoro zote  zilizoonekana. 


Aidha Mkurugenzi amemuagiza Muhandisi wa Wilaya kutengeneza BOQ zenye uhalisia na kusimamia vyema mpango kazi wa Mkandarasi anayejenga jengo la makao makuu ya Wilaya.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.