• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

HALMASHAURI KUU KUJADILI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI

Posted on: April 11th, 2023

Wajumbe wa Halmashauri Kuu  Wilaya ya Kibiti wamepokea na kuridhia utekelezaji wa ILANI ya Chama cha Mapinduzi CCM katika kipindi cha mwaka wa fedha kuanzia  julai 2022 hadi disemba 2022.

Hayo yamejiri katika kikao cha Halmashauri Kuu CCM ngazi ya Wilaya kwa lengo la kusomewa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya kibiti.

Akisoma taarifa ya utekelezaji, Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema Halmashauri imepanga kutekeleza Miradi  mbalimbali ya maendeleo yenye jumla ya sh 8,841,173,508,00 ambapo kati ya fedha hizo sh 774,186,508,00 zinatokana na mapato ya ndani ya halmashauri, sh 4,409,177,000.00 fedha za serikali Kuu na sh 3,687,810,000,00 zikitoka kwa wahisani.

Vilevile Kanali Kolombo amesema kuwa, hadi kufikia Disema 31 mwaka 2022 Halmashauri ilipokea jumla ya sh 4,188,884,239.20 sawa na 47.38% ambazo zimepangwa kutekeleza miradi mbalimbali na mpaka sasa jumla ya sh 3,030,016,969,00 ambazo ni sawa na 72%.33 zimetumika kutekeleza miradi ya Maendeleo inayoendelea kutekelezwa na iliyokwisha kutekelezwa.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya amesema katika kufikia malengo, mafanikio  ya  Wilaya ya Kibiti ni matokeo ya  vipaumbele vilivyowekwa kwenye MPANGO wa Maendeleo kwa lengo la kuendeleza na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi  katika sekta za Afya, elimu, kilim, mifugo na ushirika, maji, barabara na mendeleo ya jamii kwa kushirikisha Wadau mbalimbali  kama Koffih,Tasaf, Benki ya Dunia, TFS na NGO’S.

Akijibu hoja za wajumbe Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, ndg. Mohamed Mavura amesema kuwa, pamoja na kazi kubwa iliyofanyika Kibiti lakini yapo mapungufu madogo madogo yaliyojitokeza wakati wa ukamilishaji wa kazi hizo hivyo Mavura amewataka Wataalamu wote kila mmoja kwa nafasi yake, asimamie vizuri kazi zake ili kuhakikisha kazi zinafanyika bila mapungufu hata hayo madogo madogo na kuhakikisha Kibiti inakuwa ya mfano wa kuigwa katika usimamizi wa miradi ya maendeleo  na ustawi wa watu wake.

Aidha Mbunge wa Wilaya ya Kibiti Mhe. Twaha Mpembenwe amemtaka Mkurugenzi Mohamed Mavura kuongeza vyanzo vipya vya mapato kuhakikisha kibiti inapata mapato ya kutosha hususani katika maeneo ya visiwani (Delta) ambako kuna mazao ya hewa ya ukaa, mikoko n.k. Vilevile amewataka Madiwani, Mkurugenzi kufuatilia fedha za mfuko wa Jimbo kujua mapato na matumizi na namna zinavyotolewa.

Katika kikao hicho Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya kibiti Mhe. Juma Ndaruke  amewataka wataalamu kutumia Taaluma zao vizuri, kutekeleza miradi ya maendeleo.

“Kawajibikeni ipasavyo, kila mmoja atimize majukumu yake kulingana na nafasi yake, hii itatusaidia kufika mahali tunapotaka kufika.” Alisema Ndaruke .

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibiti Mhe. Ramadhan Mpendu amewataka wajumbe wa Halmashauri kuu kusimamia na kuilinda miradi ya Maendeleo kwa weledi kwani imebeba mabilioni ya fedha za walipa kodi wa Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.