• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

IDARA YA ELIMU MSINGI KUTEMBELEA MIRADI YA ELIMU

Posted on: April 14th, 2023

14/04/2023

Afisa Elimu divisheni ya Awali na Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Mwl. Zakayo Mlenduka ambaye ndiye Mwenyekiti wa Miradi mbalimbali inayotekelezwa Wilayani humo akiambatana na Wasaidizi wake Pamoja na Mhandisi, wamefanya ziara ya ukaguzi wa maeneo yatakapojengwa majengo mpya ya madarasa kwa Shule za  Msingi na nyumba za walimu katika Kata za Mtawanya, Mjawa na Bungu kwa ufadhili wa mradi wa Boost na  Fedha kutoka Serikali Kuu.

Boost ni Mradi endelevu wa kuimarisha ujifunzaji na ufundishaji kwa kuboresha miundombinu ya Elimu kwa shule za Awali na Msingi. Katika Wilaya ya Kibiti Mradi huu unatekelezwa katika maeneo ya Kata  mbalimbali kama Bungu, Mjawa , Mlanzi, Mtawanya, na Ruaruke.

Wakiwa katika Kata ya Mtawanya Kitongoji cha Makima wamekagua eneo la ujenzi wa nyumba mbili kwa moja za walimu wenye thamani ya sh. 50,000,000 utakao tekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu na katika shule hiyo hiyo kupitia mradi wa Boost jumla ya sh 73,000,000 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vipya 3 vya madarasa sambamba na ujenzi wa matundu 4 ya vyoo na ujenzi huo unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa mara tu fedha zitakapoingia.

Vilevile timu hiyo ambayo imeongozwa na Mlenduka imetembelea na kukagua maeneo ya ujenzi wa Shule mpya za Jaribu Magharibi na Bungu wenye thamani ya sh 306,900,000 kwa kila shule kwa ufadhili wa fedha za Boost.

Katika maeneo hayo yaliyokaguliwa kwa kila shule kutajengwa vyumba 7 vya madarasa, vyoo matundu 16, vyumba 2 vya madarasa ya awali ya mfano, Jengo la Utawala, kichomea taka, makabati na kifaa cha kuhisi moto (Smoke detector).

“Huu ni mradi mpya kabisa utakaokuwa wa mfano, tushirikiane kwa kila namna kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati na viwango vyenye ubora wa hali ya juu” alisema Mlenduka.

Hata hivyo mara baada ya ukaguzi wa kitaalam Kaimu Muhandisi wa Wilaya, Muhandisi Juma Kubadesha amethibitisha kuwa, maeneo yote aliyokagua  yanafaa kwa ujenzi. Pia amewaagiza watendaji kuhakikisha wanafanya usafi kwenye maeneo hayo, tayari kwa maandilizi ya ujenzi utakaozingatia mpangilio mzuri wa majengo na kwa kufuata michoro ya ramani elekezi.

Aidha Watendaji hao wamesema Mradi wameupokea kwa furaha kubwa, na wananchi wapo tayari kujitolea kwa ajili ya kuongeza nguvu kazi, kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.