• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

“IFIKAPO MACHI 25 MWAKA HUU, MUWE MMEHAMA MAENEO HAYA” - DC KIBITI

Posted on: March 22nd, 2024

NI KUFUATIA MAFURIKO YATOKANAYO NA MAJI YALIYOFUNGULIWA KUTOKA BWAWA LA KUFUA UMEME LA MWALIMU NYERERE.

18.3.2024

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo akiwa ameongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama, amewaagiza wakazi wa Kitongoji cha Beta Kata ya Mtunda na vijiji vyote vilivyopitiwa na delta ya Rufiji kuhamia maeneo yaliyoinuka ili kuepuka uwezekano wa uwepo wa maafa ya Mafuriko yanayotokana na maji yaliyofunguliwa katika bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere.

"Kutokana na hali ya maji ilivyo, niwatake tu muanze kuhama kuelekea katika maeneo yenye miinuko ili kuepuka maafa,  maji yanaweza kuongezeka zaidi ikawa shida kutoka na tunaelekea katika msimu wa masika" Alisema Kanali Kolombo.

Kanali Kolombo akizungumza na wakazi hao wenye kaya zaidi ya 3096 amewasisitiza kuhakikisha wanatekeleza  zoezi la kuhama haraka iwezekanavyo na mpaka kufikia  tarehe 25.3.2025 wawe wamekwisha kuhama katika maeneo hayo.

Vilevile Kanali Kolombo amewaagiza watendaji Kata wote kusimamia zoezi Hilo kwa vitendo, kwa kushiriki kikamilifu shughuli za uokoaji katika maeneo yao na kutoa taarifa zilizo sahihi, kusimamia uundwaji wa Kamati za maafa katika ngazi ya Kata, vijiji na Vitongoji kwa mujibu wa Sheria.

Hata hivyo, Diwani wa Kata ya Mtunda Mhe. Omari Twanga baada ya kufika katika Vitongoji hivyo amewataka wananchi wake kuchukua tahadhali kulingana na uhalisia wa wingi wa maji  ikiwa ni pamoja na kuhama katika maeneo hayo ili kunusuru uhai wao.

Naye Afisa Tarafa ya Kikale Ndg. Salim Malogwa amesema ngazi ya Wilaya wamekwisha weka utaratibu wa wakazi hao kupokelewa katika maeneo yaliyosalama na kuendelea na shughuli za kila siku mpaka maji hayo yatakapopungua.

Awali siku moja kabla timu ya Wataalam kutoka bwawa la Mwalimu Nyerere ambayo imeweka kambi katika Wilaya ya Kibiti na Rufiji kwa lengo la kutoa uelewa  na kuchukua tahadhari baada ya kufunguliwa maji kutoka katika bwawa hilo, walifika katika maeneo ya Beta, Nganyanga na kilindini  kutoa elimu kwa wananchi hao sambamba na kujionea hali halisi ilivyo.

"Tulitarajia bwawa litajaa kwa muda wa miaka 3 lakini limejaa ndani ya  mwaka 1 na miezi 3 na mitambo haijakamilika kujengwa hivyo inatulazimu tupunguze maji kwa kuyafungulia kupitia milango tuliyoweka kwa tahadhari ili kulinda bwawa lisibomoke" Alisema  Mhandisi Dismas Mbote.


Kauli hiyo imekuja baada kufunguliwa maji kutoka katika bwawa la Mwalimu Nyerere kuanzia machi 5 na zoezi linatarajiwa kumalizika Mei, 25 mwaka huu. Mpaka sasa kiasi cha maji kilichofunguliwa ni 3,120m3/s (sawa na lita 3,120,000 kwa sekunde).


"Tuliaza kujaza bwawa tarehe 22.12. 2022. Leo kina cha maji kimefikia mita 183.26 (kati ya 184.00) juu ya usawa wa bahari. Maji yanayoingia bwawani ni mita za ujazo 3,558.50m3/s (lita 3,558,000 kwa sekunde) na Maji tunayopunguza (spill) ni 3,120.34m3/s (lita 3,120,000 kwa sekunde). Mpaka bwawa linajaa ni mita za ujazo billioni 31.906 (lita trillioni 31). Uwezo wa mwisho wa bwawa kupokea maji ni mita za ujazo bilioni 32 (lita trilion 32) na sasa Bwawa limejaa kwa asilimia (97.33%)" Alisema Eng. Mbote.

Naye Kaimu Meneja Mazingira wa Tanesco Makao Makuu Ndg. Tluway Sappa amewasisitiza wananchi kuepuka kusubiri madhara yatokee ndiyo waanze kuhama hivyo ni vema kuchukua tahadhari mapema kuelekea nchi kavu kabla maji hayajaongezeka.


"Niwasihi tu muhame sasa, toeni vitu vya muhimu mapema ikiwa ni pamoja na kubeba vyakula, msisubiri maafa yatokee ndipo muanze kuhangaika” Alisema Sappa.


Akizungumza na wakazi wa Beta Afisa Mazingira kutoka bwawa la Mwalimu Nyerere, Ndg. Yusuph Kamote yeye amewataka wananchi hao kuwa waangalifu katika kipindi hiki kwani maji husafiri na viumbe mbalimbali kama vile mamba, viboko, nyoka wakubwa n.k hivyo ni vema kuthamini uhai wao kwa kuhama mapema kabla maafa hayajayokea.

Aidha wakazi ya Vitongoji hivyo wamesema wako tayari kutoka maeneo hayo ili kuweza kunusuru maisha yao huku wakikiri uwepo wa ongezeko la wingi wa maji tofauti na ilivyozoeleka. Mpaka sasa tayari kuna familia zimehama na nyingine zinaendelea kuhama taratibu.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.