• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

JUKWAA LA WANAWAKE KIBITI

Posted on: March 27th, 2024

25.03.2024

Diwani wa Kata ya kibiti Mhe. Hamidu Ungando amewasihi wanawake wajasiliamali  kuwa na tabia ya kuchukua mkopo kwa malengo ya muda mrefu na yenye kuleta tija na si kwa ajili ya kutunzana sambamba na kurejesha ili wahitaji wengine nao wapate fursa ya kukopa.

Awali Serikali  ilisimamisha mikopo hiyo  baada ya kusuasua kwa marejesho katika vikundi mbalimbali vilivyokopa ambapo sasa itatolewa kwa utaratibu mzuri tofauti na ilivyokuwa imezoeleka.

"Tunashukuru Mama, Mhe. Dkt. SSH Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kurejesha mikopo tena ambayo sasa itamwezesha mtu mmoja mmoja kukopa na kulipa peke yake na siyo mpaka kuwa na vikundi" Alisema Ungando.

"Awamu hii mikopo mtakayopewa haitahususha fedha bali mtapewa mahitaji unayohitaji katika biashara uliyoainisha" Alisema Mhe Ungando.

Hayo yamejiri katika kikao cha mafunzo ya  jukwaa la wanawake wajasiliamali Kata ya Kibiti kilichoandaliwa na kuratibiwa na Afisa Maendeleo ya jamii wa Kata hiyo Ndg Geoffrey  Haule kwa lengo la kuwapatia elimu na kuwajengea uwezo wa kuweza kuendesha biashara na kupata mikopo inayorejesheka yenye masharti nafuu kwa kuainisha biashara na kujiunga katika vikundi.

Afisa Maendeleo huyo amesema Dhumuni kubwa la kuwezesha mafunzo hayo ni kutoa elimu juu ya ujasiliamali, utoaji wa mikopo, utunzaji wa kumbukumbu na faida, ukuzaji na upatikanaji wa masoko kupitia mitandao ya kijamii, kupinga ukatili wa kijinsia, ndoa, mimba za utotoni na utoro mashuleni. Dhumuni lingine ni kutoa elimu ya malezi ya familia, kufanya biashara wanazopenda kwa ubunifu zinazovutia wateja kwa urahisi.

Katika kufanikisha mafunzo hayo  yenye mada mbalimbali Ndg. Haule ameshirikiana na wadau wengine wa  maendeleo kutoka Wilaya ya Kibiti ambao ni Afisa Ustawi wa jamii, dawati la jinsia, Afisa biashara, Madiwani viti maalum, viongozi wa jukwaa la wanawake, viongozi wa vyama ngazi ya Kata na Wilaya, Katibu wa chama cha walimu na makundi maalum.

Wakitoa nasaha mbalimbali kwa nyakati tofauti viongozi waalikwa wakiongozwa na Madiwani wa viti maalum wamewataka wajasiliamali hao kuhakikisha waliyofundishwa wanayafanyia kazi kwa maendeleo yao binafsi na Kibiti kwa ujumla.

Mara baada ya mafunzo kukamilika wajasiliamali hao wameonekana kuelewa na kuhamasika, jukwaa hili limekuwa na mvuto wa kipekee kutokana na namna walivyojitokeza kwa wingi ambapo kulikuwa na jumla ya wanawake 260.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.