• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KAMATI YA AFYA YA MSINGI WILAYA YA KIBITI (PHC) NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA WASH(PforR)

Posted on: December 15th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo ameongoza kikao cha kamati ya Afya ya msingi ngazi ya Wilaya ya Kibiti, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti siku ya Alhamisi Tarehe 14.12.2023

Mada kubwa iliyojadiliwa katika kikao hicho ni Mradi wa WASH (PforR). Alipokuwa akielezea kuhusu mradi huo Bw. Laban Kitule ambaye ni Afisa Afya na mwezeshaji wa kikao juu ya mradi huo alisema;

“Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti ni miongoni mwa Wilaya 8 katika mkoa wa Pwani zinazotekeleza mradi wa WASH(PforR) kwa mwaka wa fedha 2023/2024”.

Bw. Kitule alieleza kuwa Wilaya ya Kibiti imepokea kiasi cha fedha Jumla ya Tsh. 238,848,519.12 kama mbegu kwaajili ya utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya vyoo katika vituo 5 vya kutolea huduma za Afya ambavyo ni zahanati 4 na Kituo cha Afya 1.

Vituo hivyo ni: Zahanati ya Ruaruke, Zahanati ya Rungungu, Zahanati ya Bungu, Zahanati ya Mchukwi pamoja na kituo cha Afya Kibiti.

Bw. Kitule aliendelea kueleza kuwa lengo la mradi huo ni:

  • Kuboresha miundombinu ya maji na usafi wa mazingira katika vituo vya huduma za Afya.
  • Kuhamasisha ujenzi na matumizi ya vyoo bora katika ngazi ya kaya pamoja na kuhimiza tabia ya kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni.
  • Kuongeza idadi ya vijiji ambavyo vimefikia hatua ya daraja la juu la usafi kwa kuhakikisha kaya zote zinakuwa na vyoo bora na kuondoa kabisa tabia ya kujisaidia hovyo.
  • Kuboresha ukusanyaji wa taarifa sahihi za usafi wa mazingira katika kaya na taasisi kwa kila robo ya mwaka.

Mpaka sasa shughuli ambazo zimeshatekelezwa ni kuhamasisha ujenzi wa vyoo bora ngazi ya kaya na Kujenga miundombinu ya usafi wa mazingira katika Zahanati na Kituo cha Afya.

Aidha kwa kutekeleza vyema mradi huu Halmashauri, Vituo na Kaya zote zitanufaika kama ifuatavyo:

  • Ikiwa kutakuwa na ongezeko la idadi ya kaya zenye vyoo bora kwenye taarifa za mwaka zinazoripotiwa basi kila kaya italipwa dola 3 za kimarekani kwa mwaka.
  • Kukiwa na ongezeko la idadi ya vijiji kufikia kiwango cha juu cha usafi wa mazingira, Wilaya italipwa dola za kimarekani 16,000 kwa mwaka.
  • Wilaya italipwa dola za kimarekani 24,000 kwa mwaka kama itatuma taarifa za robo kwa wakati, usahihi na ukamilifu kwenye usafi wa kaya na vituo vya Afya.
  • Kukiwa na ongezeko la idadi ya vituo vilivyoboresha miundombinu ya vyoo na usafi wa vituoni kila kituo kitakachokidhi kigezo kitalipwa dola za kimarekani 29,000.

Akichangia kikao hicho Kanali Kolombo ameishukuru serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa za kuleta maendeleo nchini lakini pia kujali Afya za Wananchi wake kwa kutuletea miradi kama hii.

Kanali Kolombo aliongeza kuwa mradi huu ni muhimu hivyo unahitaji uhamasishaji na uelimishaji wa kutosha kwa wananchi ili uweze kutekelezwa na kuleta tija kama ilivyokusudiwa.

Akieleza juu ya mikakati iliyopo Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Elizabeth Oming’o amesema Idara ya Afya tayari imeshachukua hatua ya Kuelimisha Umma juu ya umuhimu wa choo bora kupitia Maafisa Afya waliopo pamoja na wenyeviti wa vijiji kwa maeneo yatakayopitiwa kama mfano wakati wa ukaguzi.

Maeneo hayo ni Kata ya Bungu pamoja na Kibiti hivyo anawasisitiza Wananchi wote hususani wa maeneo tajwa kudumisha usafi sio wa vyoo tuu bali ni pamoja na mazingira yanayowazunguka.


Naye Diwani wa Kata ya Kibiti Mh. Hamidu Ungando alisema, mradi huu ni muhimu sana sio kwasababu utawapatia kaya husika fedha lakini utaepusha magonjwa ya mlipuko ambayo serikali hutumia gharama nyingi sana kukabiliana nayo badala ya kutumia fedha hizo kuleta maendeleo.

Akimalizia kuchangia kikao hicho Sheikh Thabit Milindo wa Wilaya ya Kibiti alisema usafi ni muhimu mno hata vitabu vya dini vinasisitiza hilo, ndiyo maana hata mahali wakitaka kujenga Msikiti wanaanza kujenga kwanza choo.

Kanali Kolombo ametoa rai kwa Wananchi wote wa Wilaya ya Kibiti kuhakikisha kuwa kila kaya inakuwa na choo bora lakini pia wafanye matumizi sahihi ya vyoo hivyo.

“Hakutakuwa na maana ikiwa watu wamejenga vyoo bora lakini bado wanajisaidia vichakani, msijenge vyoo kama mapambo, jengeni na mvitumie ili kuweka safi mazingira yetu” Alisema Kolombo

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.