• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya kibiti imefanya ziara ya kukagua miradi yenye thamani ya Shilingi 146,700,000.00 tarehe 31.01.2024

Posted on: February 2nd, 2024

Kamati hiyo ilipita na kukagua miradi ifuatayo:

1.Ujenzi wa nyumba za Walimu 2 kwenye jengo moja (2 in 1) katika shule ya Msingi kikale inayojengwa kwa kutumia MAPATO YA NDANI mpaka sasa Halmashauri imepeleka Tsh. 18,600,000.00, ujenzi umefikia hatua ya kupaua.

2.Ujenzi wa matundu ya Vyoo, Kinawia mikono, Mnara wa maji na Kichomea taka katika Zahanati ya Rungungu, mradi umekamilika kwa kutumia Tsh. 37,700,000.00 ambazo ni fedha za SANITATION.

3.Kiwanda cha Ukamuaji wa mafuta ya mawese kinachoendeshwa na Kikundi cha Vijana Uchumi Ruaruke A ambacho kimewezeshwa kwa kupewa Mkopo wa Tsh. 20,000,000.00  na Halmashauri kutoka kwenye MAPATO YA NDANI, Kiwanda kimekamilika lakini kinafanya kazi kwa kusuasua.

4.Mashine ya Kusaga na kukoboa nafaka inayoendeshwa na kikundi cha Tushikamane Nyamatanga. Kikundi kimewezeshwa kwa kupewa Mkopo wa Tsh. 10,000,000.00 na Halmashauri kupitia MAPATO YA NDANI. Mashine imekamilika na inafanya kazi vizuri.

5.Ujenzi wa shule ya sekondari ya Wananchi katika Kata ya Kibiti, mpaka sasa imetumia Tsh. 38,000,000.00 ambayo ni nguvu ya wananchi kujenga maboma ya madarasa 4 na katika kuunga mkono juhudi hizo za wananchi kwenye ukamilishaji MFUKO WA JIMBO umetoa Tsh. 5,400,000.00 na Halmashauri imepeleka Tsh. 10,000,000.00 kutoka kwenye MAPATO YA NDANI, Ujenzi upo kwenye hatua ya umaliziaji wa maboma ili kupaua.

6.Biashara ya huduma za kifedha na gesi inayoendeshwa na Bi. Zainabu Kwangaya ambaye aliwezeshwa kwa kupewa mkopo wa Tsh. 7,000,000.00 kutoka kwenye MAPATO YA NDANI. Biashara hii inaendelea vizuri.

Baada ya kuiona miradi yote wajumbe walitoa mapendekezo yao kwenye majenzi yote yaliyokamilika na yanayoendelea kwa kumtaka Mhandisi kufanya marekebisho haraka kabla ya kuendelea na shughuli zingine ambapo hitilafu ndogondogo kwenye kuta ndiyo tatizo lililoonekana Zaidi.

Kwa kikundi cha Vijana Uchumi Ruaruke A, kamati ilisimama kidete kuwa ni lazima kikundi hicho kirejeshe fedha hizo kwakuwa walichopewa kilikuwa ni mkopo na sio msaada.

“Vijana wetu tumewasikia, pamoja na changamoto mlizokutana nazo kwenye biashara yenu lakini bado ni lazima mzilipe fedha hizo. Mlichopewa kilikuwa ni mkopo na sio msaada, hizo ni fedha za Wananchi wa Kibiti hivyo ni lazima zirejeshwe ili na wengine wanufaike nazo” Alisema Mh. Omari Twanga ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo.

Kwa Kikundi cha Tushikamane, Kamati ilisema imesikia maombi yao hivyo, wameyachukua na wanakwenda kujadili kwenye vikao vyao wanaamini maombi yao yatafanikiwa kwakuwa wameonesha nia ya dhati ya kurejesha mkopo wao.

Kikundi cha Tushikamane kiliomba kuongezewa muda wa marejesho kwakuwa walishindwa kufanya kazi kwa muda lakini sasa wanaendelea vizuri na wamekwisharejesha sehemu ya mkopo huo.

Aidha Kamati imemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan kuendelea kuunga mkono juhudi za wananchi kwa kuwaletea Tsh. 350,000,000.00 ili kukamilisha maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi na kuongeza majengo mengine ili shule hiyo ikamilike.

Kamati ilihitimisha ziara yake katika duka la Bi. Zainabu Kwangaya ambaye anaendelea vyema kutoa huduma za kifedha na uuzaji wa vifaa vya simu na gesi. Kila mmoja alimsifu mama huyo kwa ujasiri alionao kwakuwa licha ya ulemavu wa viungo alionao bado anaendelea kuipambania familia yake kwa kuendesha biashara yake na kufanya marejesaho vizuri, hivyo wanategemea akimaliza mkopo huo atachukua mwingine mkubwa zaidi ili aendelee kupanua biashara yake.

Kwa upande wake Bi. Zainabu amesema anamshukuru sana Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Mbunge wa Kibiti, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti pamoja na Diwani wake wa Kata ya Kibiti kwa jitihada zao za kuhakikisha makundi maalum yanainuka na kujitegemea kiuchumi. Mikopo wanayopewa imewasaidia sana kujitegemea. 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.