• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KAMATI YA MAAFA WILAYA YA KIBITI YAWEKA MIKAKATI YA KUJIHAMI NA MVUA ZA EL-NINO

Posted on: October 3rd, 2023


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Bw. Hemed Magaro amefungua kikao kazi cha kamati ya uratibu  wa Maafa ya Wilaya ya Kibiti chenye lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kukabiliana na mvua za el -nino zinazotarajiwa kuanza mwezi huu nchini ambazo zinaweza  kuweza kusabanisha Maafa katika maeneo ya mabondeni wilayani Kibiti.

" Tumepokea taarifa ya uwezekano wa uwepo wa maafa yatokanayo na mvua za elnino katika mikoa 14 Tanzania ikiwemo na Mkoa wa Pwani." Alisema Hemed Magaro.

Katika kikao hicho Mkurugenzi Hemed  Magaro amewataka Wajumbe walioshiriki kikao hicho kuitikia wito mara wanapoitwa kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao muda na wakati wowote pindi watakapohitajika katika zoezi la maafa.

" Niwaombe , muwe tayari kuitikia wito wakati wowote mtakapohitajika, nyie ni Kamati ya Wataalam ya maafa, tunategemea maelekezo yenu" Alisema Magaro.

Vilevile  Magaro amesema katika kuhakikisha wanakabiliana  na janga hilo wameweka mikakati mbalimbali itakayosaidia kutekeleza usimamizi wa maafa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kupitia njia mbalimbali ili jamii iweze kupata uelewa wa nini kinaweza kutokea na namna ya kujiokoa.

Vilevile amesema mikakati mingine waliyoweka Kwa pamoja wameaximia kuhakikisha kunakuwepo na vifaa vya kutosha vya uokoaji sambamba na rasilimali watu, kuandaa bajeti ya dharura ya maafa, kutoa njia za mawasiliano, kujua idadi ya watu wanaoishi katika  maeneo hatarishi  n.k

Hata hivyo Magaro ameagiza idara ya afya kuhakikisha kunakuwa na akiba dawa  za kutosha hasa kipindi hiki tunachotarajia mvua za el nino kuanza kunyesha. Pia amesisitiza vyombo vya usafiri majini na nchi kavu vikarabatiwe na viwe tayari wakati wowote kuanzia sasa.

Mbali na hayo, Mwenyekiti Magaro ameagiza idara ya kilimo kuandaa mbegu za mazao ya muda mfupi kutumika kupunguza changamoto ya chakula baada ya mafuriko kutokea kwani kitaalamu maeneo yanayopitiwa na mafuriko hustawisha sana chakula katika ukanda wa  bonde la mto Rufiji.

Naye Mratibu wa Maafa Wilaya ya Kibiti Bw. Gideon Zakayo amesema katika Wilaya ya Kibiti maeneo ambayo  wananchi wanaweza kuathiriwa na mvua za elnino ni katika Kata ya Mtunda maeneo ya Nyambele, Nganyanga, beta, mbwanga na kifimbo, Kata ya maparoni ni maeneo ya usimbe kiwanjani,gingi,mbangani na usimbe kidoga, na  Kata ya mbuchi ni maeneo ya kipoka, mikwang'ombe, barabarani na kumbacha wakati katika Kata ya msala ni  tarachu na domwe kwani maeneo haya yapo bondeni mwa mto Rufiji hata mvua za mwaka 2020 zilileta athari kwa maeneo hayo..

Aidha  Mratibu wa maafa Zakayo amesema katika kipindi hicho maeneo ambayo wananchi wanaweza kuhamia  kujisitiri  katika Kata ya Mtunda ni Kijiji cha Mtunda A, Kata ya mbuchi maeneo salama ni nganje na kitingi, Kata ya msala ni kisimbya na twasalie wakati huo huo Kata ya Ruaruke na kikale ni yameonekana kuwa maneno salama zaidi katika misimu yote wilayani kibiti.

Katika kikao hicho SGT. Boniface Kijumbe kutoka kikosi cha zimamoto Wilaya ya Mkuranga amesisitiza Taasisi ya Tarura Wilaya ya Kibiti kwa kushirikiana na Maafisa wa Idara ya Afya na Mazingira kuhakikisha taka hazirundikwi au kutupwa hovyo, kuzibua mitaro na kuhakikisha wanatengeneza njia za dharura ili mvua zitakapoanza kunyesha takataka zisizuie maji kupita Kwa urahisi.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.