• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KAMATI YA SIASA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KIBITI

Posted on: March 26th, 2023


Kuhakikisha Miradi inaendana na thamani ya fedha kwa  kuzingatia viwango.

Waakuu wa idara na wasimamizi wa Miradi mbalimbali katika sekta za Umma Wilaya ya Kibiti, wametakiwa  kuongeza umakini katika utekelezaji na ufuatiliaji wa Miradi inayotekelezwa kwa kuwajibika ipasavyo ili iweze kuleta tija kwa maendeleo ya Kibiti.

“Mkawajibike kutimiza majukumu yenu kama kanuni zinavyoelekeza, mliopo hapa mmeaminiwa kusimamia idara mlizopo, kila mmoja akajitume kuitendea haki nafasi aliyoaminiwa kuitumikia” Alisema Mhe. Ndaruke.

Hayo yamejiri katika ziara ya kamati ya Siasa Wilaya ilipotembelea na kukagua baadhi ya Miradi ya maendeleoinayotekelezwa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 kwa lengo la kujionea hali halisi, Pamoja  na kuongeza ufanisi.

Hata hivyo kamati imeiagiza idara ya manunuzi kununua vifaa kwa wakati ili kazi ya ujenzi iendane na muda uliokusudiwa kukamilisha Miradi husika.

Vilevile kamati  ya Siasa imewataka Wataalam,wasimamizi,na Wakuu wa Idara, kujiridhisha katika kila hatua ya Mradi mapema kabla ya kwenda hatua nyingine ili kuepuka gharama za marekebisho ya makosa madogo madogo ya kiufundi hatimaye fedha zilizopangwa ziweze kukamilisha Miradi .

“Kabla ya kupiga hatua nyingine katika Miradi Wataalam piteni kujiridhisha, ndipo hatua nyingine ianze ili kuepuka kupata hasara ya kuongezeka kwa gharama”Alisema Mwenyekiti Ndaruke.

Mbali na hayo kamati imesisitiza jitihada zifanyike kwa taasisi zinazotoa huduma kwa jamii ili kuimarisha Miundombinu ya Maji, Barabara na Umeme kwani bado ni changamoto katika maeneo mengi ya miradi jambo linalosababisha kuchelewesha maendeleo .

Pia Kamati hiyo imewaasa Watumishi wa umma na taasisi zote kutumia lugha nzuri katika maeneo ya kazi, kuwajali wananchi wanaowatumikia, kujituma ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutekeleza mikakati iliyopangwa kwenye miradi inayoendelea na inayotarajiwa kuanza.

Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya Bw. Juma Ndaruke ambayo iliambatana na viongozi mbalimbali wa Wilaya ikiwa ni  pamoja na Wakuu wa Idara na vitengo, wakuu wa Taasisi za Umma  ilinzia katika kituo cha Nyamatanga kata ya Ruaruke ambapo  walikagua ukarabati wa jengo la OPD, ujenzi wa maabara, Jengo la upasuaji, Jengo la kujifungulia, na Jengo la kuhifadhia maiti ambapo jumla ya sh 446,006,356.28 fedha za Serikali Kuu kupitia TASAF zimepangwa kutumika.

Ziara ikaendelea katika Hospitali ya wilaya ambapo walikagua uendelezaji wa ujenzi wa jengo la upasuaji, wodi ya upasuaji kwa wanawake na wanaume pamoja na Jengo la kuhifadhia maiti ambapo jumla ya sh 800,000,000 fedha  kutoka serikali kuu zinatumika Pia walikagua ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharura lenye thamani ya sh 300,000,000  fedha za Uviko, kutoka Serikali Kuu.

Katika ziara hiyo pia walifika katika Kata ya Bungu kwenye mradi wa shule ya sekondari ya Nyambili Nyambunda yenye ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa na ofisi ya walimu wenye jumla ya sh 100,000,000, kwa fedha za serikali kuu,ambapo ujenzi umekamilika na madarasa yameanza kutumika.

Mbali na miradi hiyo pia walitembelea Kata ya Mjawa kukagua ujenzi wa shule ya sekondari ya jaribu mpakani -SEQUIP iliyojengwa kwa fedha za serikali kuu (tozo za miamala ya simu) zenye jumla ya sh 470,000,000 na mapato ya ndani sh 30,231,000. na Kisha kukamilisha ukaguzi huo katika kituo cha afya Mjawa ambacho kinaendelea na ukamilishaji wa baadhi ya majengo huku kikiwa kinaendelea kutoa huduma za kitabibu.

Akiishuru kamati ya siasa, Mkuu wa Wilaya ya kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema ziara na kikao kilichofanyika ni faida kwa Wataalam kwani kinawakumbusha Wakuu wa Idara kutekeleza ilani ya chama Tawala na kufuata miongozo ya kazi.

Nae kaimu Mkurugenzi Mtendaji  Mwl. Zakayo Mlenduka amesema kupitia ziara hiyo maagizo na changamoto zote zilizotolewa amezipokea na kuahidi kuzifanyia kazi kadri itakavyowezekana ili kuhakikisha malengo yanatimia.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.