• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KAMATI YA SIASA WILAYA YA KIBITI YATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO.

Posted on: August 13th, 2024

12.08.2024

Kamati ya Siasa Wilaya ya Kibiti ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Juma K. Ndaruke imefanya ziara ya kutembelea na kukagua baadhi ya miradi ya maendeleo iliyotekelezwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Jumla ya Miradi 6 yenye thamani ya shilingi 631,802,640.00 imekaguliwa. Miradi hiyo ni Ujenzi wa chumba 1 cha darasa Shule ya Sekondari Dimani, Ujenzi wa Bweni la watoto wenye mahitaji maalumu Shule ya Msingi Kitundu, Ujenzi wa Shule na Umaliziaji wa vyumba 4 vya madarasa Shule Tarajiwa ya Sekondari ya Wananchi Kibiti, Ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa na matundu 5 ya vyoo Shule ya Msingi Msafiri, Ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa Shule ya Msingi Kinyamale na Umaliziaji wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya Sekondari Jaribu.

Mhe. Ndaruke amesema ziara hiyo ni ya kawaida na lengo lake siyo kutafutana nongwa bali ni kuona kazi zinazotekelezwa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi zimesimamiwa ipasavyo ili kuleta tija, pa kukosolewa pakosolewe na pa kupongezwa papongezwe.

Wakiwa kwenye ziara hiyo, Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Kibiti wamepongeza sana Uongozi wa Halmashauri (Mhe. Mkuu wa Wilaya, Wahe. Madiwani, Katibu Tawala, Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Wataalamu wote) kwa kazi nzuri ya usimamizi wa miradi hiyo kwani kote walikotembelea majengo yapo vizuri.

Aidha Kamati imesisitiza Samani zinazonuliwa kwaajili ya miradi hiyo ziendane na ubora wa majengo yaliyopo ili hadhi na thamani ya fedha zilizotumika ionekane.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg. Hemed Magaro ameishukuru kamati kwa pongezi walizotoa baada ya kuona jitihada za Wataalamu kwenye usimamizi wa miradi hiyo, naye akitoa pongezi kwa Kamati hiyo kwani nao wanapambana sana ili Halmashauri ipate fedha za miradi huku akiahidi kufanyia marekebisho changamoto ndogondogo zilizoonekana.

Akihitimisha ziara hiyo Mh. Ndaruke amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha kwaajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo Kibiti, Uongozi wa Mkoa, Wilaya pamoja na Wananchi wa Kibiti kwa kusimamia vyema miradi hiyo.

“Niwashukuru sana wote mliohusika kwenye usimamizi wa miradi hii kwani mmesimamia vyema utekelezaji wa Ilani ya Chama, hivyo sisi Wanasiasa tuna maneno mengi ya kusema huko kwenye majukwaa kwa kazi hii kubwa mliyoifanya” 

“Lakini pamoja na pongezi hizi nyingi mlizopata msiende kubweteka, ukisifiwa maana yake mazuri ni mengi kuliko mabaya kwahiyo mkaendeleze haya mazuri mliyioanzisha” Alisema Ndaruke.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.