• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AITAKA HALMASHAURI KUWAKUMBUKA WATOA HUDUMA WA VIJIJI (WAVI)

Posted on: July 11th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Kibiti kanali Joseph Kolombo ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kuwakumbuka watoa huduma wa vijiji (Wavi) ambao husaidia kutoa huduma, kufuatilia na kuripoti taarifa za hali ya lishe ya vijiji.

Hayo yamejiri leo Julai 11, 2024 katika kikao cha tathmini ya Mkataba wa lishe ngazi ya Kata kwa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo moja ya changamoto iliyowasilishwa na Afisa lishe Wilaya ni ucheleweshwaji wa taarifa kutoka kwa watendaji kata ambao nao walisema wanapata changamoto kupata taarifa hizo kutoka kwa WAVI kwani wanaonekana kutojali uharaka wa taarifa hizo kwakuwa imekuwa ni kazi ya kujitolea zaidi kwao bila malipo.

“Mkurugenzi naomba ulichukue hili, muwafikirie hawa WAVI kwakuwa ni watu muhimu sana ambao wanatusaidia kule vijijini” Alisema Kanali Kolombo.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Bw. Denis Kitali amesema kwakuwa jambo hilo limekaa kibajeti zaidi Halmashauri imelichukua na litashughulikiwa kwahiyo WAVI wawe na subira na waendelee kutoa huduma.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe kwa robo tatu, Afisa lishe Wilaya Bi. Roina Daza amesema kitengo cha lishe wilaya kimefanikiwa kufanya shughuli zifuatazo: Kutembelea na kutoa Elimu ya lishe kwenye Vijiji, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na gereza la Mng’aru. Kufanya usimamizi shirikishi katika vituo vya kutolea huduma za Afya na kutembelea na kutoa matibabu kwenye familia zenye watoto wenye hali mbaya ya lishe.

Aidha Bi. Roina pia amesema hali ya lishe kwenye kata zote imeendelea kuimarika, 98.9% ya vijiji vimefanikiwa kufanya siku ya lishe ya Kijiji (SALIKI), 97.98% ya shule zinatekeleza mpango wa chakula mashuleni, idadi ya watoto wenye utapiamlo mkali imepungua huku kukiwa hakuna kifo cha mjamzito kilichotokea kwa robo husika. 

Akifunga kikao hicho Kanali Kolombo amewataka Watendaji wote kwenda kutekeleza na kusimamia yote waliyokubaliana ikiwemo kutoa taarifa za hali ya lishe ya Kata zao kwa wakati ili kusaidia kufanikisha lengo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha kuwa huduma za lishe zinaendelea vizuri katika maeneo yetu.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.