• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AMALIZA MGOGORO WA ARDHI MAGOGO MATA.

Posted on: July 20th, 2023


Hatimaye mwaronaini wa mgogoro wa ardhi kati ya shule ya sekondari ya wavulana Kibiti na wa magogo matatu katika Kata ya Mtawanya umepatikana baada ya pande zote mbili kuridhiana kwa kutumia mipaka ilivyotumika mwaka 2012 kupanga maeneo hayo.

Akisoma makubaliano yaliyofikiwa katika mgogoro huo, Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema, muafaka umepatikana kwa kufuata maelekezo ya mpango wa Serikali ambao umesimamia maslahi ya pande zote mbili.

Kanali Kolombo amesema kwa mujibu wa maelekezo ya mpango huo, mipaka iliyowekwa mwaka 2012 ifuatwe na kuimarishwa na wananchi wa magogo matatu wataendelea kuishi katika maeneo yao na kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo.

"Leo tumemaliza mgogoro huu, ni wakati wenu sasa kufanya maendeleo hapa na kutenga maeneo ya huduma za kijamii, kama shule na zahanati" Alisema Kolombo.

Vilevile Kanali Kolombo ameziagiza Taasisi za maji na umeme Wilaya ya Kibiti, kufanya upembuzi yakinifu na kuhakikisha wanawafikishia huduma hizo wananchi wa magogo matatu.

Hata hivyo Diwani wa Kata ya Mtawanya Mhe. Malela Tokha, amempongeza Kanali Kolombo kwa kumaliza mgogoro huo kwa muda mfupi huku akimwomba Mkuu huyo wa Wilaya kusaidia zoezi la uwekaji wa mawe ya msingi na mipaka kufanyika kwa haraka ili kuepuka matatizo kujirudia.

"Mhe. Mkuu wa Wilaya kwa niaba ya wananchi tunakupongeza sana ila tunaomba utusaidie zoezi la uwekaji mawe ya msingi na mipaka lifanyike kwa haraka, tuwe huru kufanya maendeleo yetu" Alisema Mhe. Malela.

Aidha Mwenyekiti wa Kamati ya ufuatiliaji Mzee Rashid  Musa Mkinga amesema mbali na mgogoro huo kuisha kwa amani, ameomba Kijiji cha Magogo matatu kipewe maandishi na nakala ya Ramani kama sehemu ya uthibitisho wa kuishi maeneo hayo kihalali.

" tunaomba tupewe barua yenye  maandishi ya kumalizika kwa mgogoro huu na nakala ya Ramani ambayo inathibitisha  uhalali wa kuwepo eneo hili, ikawe sehemu yetu ya ushahidi endapo itatokea sintofahamu" Alisema Rashid Mkinga.

Mwisho Mzee Rashid Mkinga amewataka wananchi wa Kitongoji cha magogo matatu kuchangamkia fursa kwa kutenga maeneo ya miundombinu ya kijamii kama vile kutenga maeneo ya shule na zahanati kwa maendeleo yao wenyewe n.k.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.