• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AMETUA UCHEMBE

Posted on: February 14th, 2023

Mkuu wa wilaya ya kibiti Kanali Joseph Kolombo amewaagiza watendaji wa vijiji, Mtendaji wa Kata ya Mjawa  na Afisa kilimo wa wilaya kupata takwimu za wakulima na wafugaji wote ikiwa ni pamoja na idadi ya mifugo ili kuweza kurahisisha zoezi la  kutenga maeneo ya ufugaji na kilimo sambamba na kutambua maeneo yaliyo wazi.

“Nahitaji kupata takwimu ya wakulima ,wafugaji na idadi ya mifugo ili tuweze kuwatengea maeneo ya kudumu, Mtendaji Kata na Afisa kilimo nendeni kwa wafugaji mkapate takwimu sahihi za mifugo na wafugaji ili tujue namna ya kuwatafutia maeneo ya kuchungia” Alisema Kolombo.

Hayo yamejiri katika kikao cha wakulima na wafugaji katika Kijiji cha Uchembe Kata ya Mjawa ambapo wakulima wamewalalamikia wafugaji kulisha mifugo katika mashamba na wakati huo huo wafugaji pia wamedai kukosa maeneo ya malisho kwasababu wakulima wamelima mpaka kwenye maeneo ya kuchungia jambo linalosababisha wao kuhangaika kutafuta maeneo ya malisho.

“Ni kweli tunapita kutafuta maeneo ya malisho kwani wamelima mpaka maeneo tunayolishia mifugo yamebaki maboma tu.”alilalamika mwakilishi wa wafugaji Bw. Ninini Mgusa.

Akiwa kijijini hapo Mkuu wa Wilaya Kanali Kolombo ametoa maelekezo kwamba kila mkulima alime eneo lililotengwa kwa kilimo na mfugaji achunge katika eneo lililotengwa kwa ajili ya ufugaji vinginevyo ni kukiuka kanuni taratibu na Sheria zilizopo.

“wakulima ,wafugaji nyie wote ni watu wangu,sipendezwi hata kidogo na malumbano yanayotokea, muheshimiane na kupendana” Alisema Kolombo.

Mbali na kero hizo amewataka wakulima kulima kwa wingi ili wapate mazao ya kutosha sambamba na kutoa taarifa endapo kutatokea tatizo na kuwataka  wafugaji waendelee kufuga katika maeneo waliopangiwa kulisha wakati serikali inatafuta maeneo maalum kwa ajili ya malisho. Pia ameagiza kukamatwa kwa  mkulima au mfugaji yeyote atakayekiuka sheria zilizowekwa.

“tutawaondoa wafugaji hapa baada ya kupata takwimu na maeneo maalumu ya kulishia mifugo yao na baada ya hapo  kwa yeyote atakaye kiuka  makubaliano haya tutamwajibisha ipasavyo” Alisema Kolombo.

Vilevile amewataka wakulima kutumia msimu huu wa mvua vizuri kwa kuhakikisha wanalima mazao ya kutosha ili kuweza kuvuna kwa wingi.

Aidha Kanali Kolombo ametembelea na kukagua shule ya sekondari Jaribu mpakani, kituo cha Afya Mjawa na Hospitali ya wilaya na kwa nyakati tofauti amesisitiza kuhakikisha miundombinu muhimu         (maji,umeme na vyoo) inapatikana kwa haraka ili  kuweza kurahisisha utoaji wa huduma kwa ufasaha .

Naye Afisa kilimo, mifugo, uvuvi na ushirika Ismail Bainga amewasihi wakulima katika kipindi hiki kuhakikisha wanatumia dawa/viwatiifu kuangamiza wadudu wanaoshambulia mpunga na mazao mengine .

Naye mkuu wa polisi wilaya ya kibiti (OCD) amewasihi wananchi wa Uchembe kutoa ushirikiano wa kiusalama katika maeneo yao, kutii sheria bila shuruti, kutoa taarifa Kwa wakati na usahihi na kuepuka kujichukulia sheria mkononi huku akikemea suala la ndoa katika umri mdogo na mimba za utotoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.