• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KIBITI YAPATA NEEMA, CHUO CHA VETA KUJENGWA KIJIJI CHA NYAMBILI

Posted on: May 23rd, 2023


MKUU wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amekutana na Wananchi wa Kijiji cha Nyambili Wilayani humo kwa lengo la kuwatambulisha  rasmi mradi mpya wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA chenye thamani ya sh bil.3.5.

"Hii ni bahati wakazi wa Nyambili Kata ya Bungu mmependelewa kwani watoto wenu watapata ujuzi katika chuo hiki,mkilinde" Alisema Kanali Kolombo.

Mradi huo unaotarajiwa kuanza mwezi Juni mwaka huu utakuwa ni msaada mkubwa na mkombozi kwa vijana wa Wilaya ya Kibiti na maeneo mbalimbali kwani chuo kitakuwa na uwezo wa kupokea vijana wengi kwa wakati mmoja.

“Mradi utaanza hivi punde, Sisi ni wasimamizi na watekelezaji wa mradi huu na miradi mingine yote inayotuzunguka “alisema Kanali Kolombo kwa msisitizo huku akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan kwa kuitazama kibiti kwa jicho la tatu na kuipatia fedha za ujenzi wa chuo cha Veta.

Kanali Kolombo amesema lengo la Serikali kuanzisha chuo cha Veta ni kuisaidia Vijana ambao hawakubahatika kuendelea na masomo ya Sekondari na chuo, kuweza kupata ujuzi na kuweza kujitegemea wa kufanya shughuli mbalimbali kulingana na fani watakazochagua kujifunza ili kujikwamua kimaisha.

Vilevile Kanali Kolombo amesema ili kukamilisha ujenzi huo kwa wakati kuna kila sababu ya kutoa ushirikiano ili kazi iweze kwenda kwa kasi, kwani kuna baadhi ya miundombinu itapita mashambani kwenu wananchi, kama vile barabara, umeme, maji  n.k.

" Ninaomba ridhieni maeneo yenu ambayo mradi utapita, ili tuweze kurahisisha kukamilika kwa mradi ninaomba ushirikiano wenu tusiupoteze huu mradi" Alisema Kanali Kolombo.

Ni matarajio yetu kama ilivyo ada mara baada ya kukamilika kwa ujenzi huu, Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan atakuja kuzindua chuo chetu, hivyo wananyambili jiandaeni kwa ugeni huo mkubwa.

Wakiwa kijijini hapo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ndg. Denis Kitali amewataka wananchi na Viongozi wa Wilaya kujitoa kusimamia kwa umakini mradi huo, kulingana na thamani ya fedha iliyotolewa kwa maendeleo ya Kibiti.

Aidha, Mkuu wa chuo cha Ufundi Ikwiriri Bi Ranalda Kyaruzi ambae ndiye Msimamizi wa ujenzi wa chuo hicho, amewataka wananchi wa kibiti kumpa ushirino kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa. Hakuishia hapo pia amewataka wazazi kuwapeleka watoto/vijana wao chuoni ili waweze kupata ujuzi wa fani mbalimbali kwani Veta imesheheni fani kedekede kama vile ujenzi, ushonaji, upishi, umeme wa majumbani n.k

Naye Mratibu wa Elimu Kata ya Bungu Mohamed Mtuliakwako amesema amefurahishwa na taarifa ya mradi na wananyambili wameupokea huku akimpongeza Mbunge wa Jimbo la kibiti Mhe.Twaha Mpembenwe kwa jitihada anazozifanya kuwasemea Wana kibiti hatimaye VETA itajengwa Wilayani Kibiti.

Mwisho wakazi wa Nyambili wakamtoa DC hofu na kumwahidi kuwa, wameupokea na watausimamia mpaka ukamilike. Kuja kwa mradi huu kutasaidia watoto wetu kuacha kuhangaika na masuala ya ajira,tumefurahi Sana .

"Uwezo wa kujitolea tunao, wananyambili ni JADI yetu kujitolea, tunapenda maendeleo chuo kinakwenda kujengwa kwa nguvu zote" Walisema baadhi ya wakazi wa Nyambili Wakiwa na nyuso za furaha wakiwawakilisha wenzao.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.