• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KIBITI YAREJESHA HISTORIA, KILIMO CHA PAMBA RASMI MSIMU HUU.

Posted on: February 15th, 2024

Hatimaye zao la pamba limerejea Wilaya ya  Kibiti kama ilivyokuwa awali ambapo ndilo lilikuwa zao kuu la biashara kabla ya kuimarishwa kwa mazao ya korosho na ufuta. Zao hilo lilipotea kutokana na kulishambuliwa na wadudu na uhaba wa masoko katika miaka ya 1980.

Katika kuhakikisha  zao hilo linarejea Jumatatu ya tarehe 12.2.2024  Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amezindua rasmi semina elekezi kwaajili ya kilimo cha pamba Wilayani humo akisema kwamba ni wakati wa Wilaya ya Kibiti kuinuka na kukua kiuchumi.

"Nimefarijika sana kuongezeka kwa zao hili katika Wilaya yangu, sasa kutakuwa na mazao manne ya biashara, kwetu sisi Wanakibiti hii ni neema" Alisema.

Kuongezeka kwa mazao ya biashara kutafanya wakulima kuwa na mzunguko mzuri wa uzalishaji bila kupumzika katika msimu sahihi wa kilimo ukiachilia mbali zao la korosho na ufuta ambayo ni muhimili wa mapato ya Wilaya, hivi karibuni tumeanzisha kilimo cha mbaazi na sasa tunakwenda kuanzisha kilimo cha zao la pamba.

Semina hiyo ililenga kutoa Elimu juu ya Kilimo cha Pamba pamoja na kuwapa ridhaa wawekezaji walioomba kuwezesha kilimo hicho Wilayani Kibiti. Hivyo Kanali Kolombo amewataka wakulima ambao wako tayari kwa kilimo hicho kuchangamkia fursa hiyo kwa kujiorodhesha majina yao tayari kwa kuanza kilimo cha pamba katika msimu huu bila kuchelewa, kwani mwekezaji amekuja na utaratibu mzuri wa uzalishaji.

"Nimefurahi sana kusikia mwekezaji atawalimia wakulima mashamba yao, atatoa mbegu na kusimamia masoko kwa kuwekeana mikataba na mkulima ambapo mwisho wa siku mkulima atakatwa pesa ile baada ya pamba kuuzwa.


Akimkaribisha Mwekezaji kutoka India Kanali Kolombo amemthibitishia kuwa Kibiti ni eneo salama kwa kilimo, ardhi yake inarutuba ya kutosha, na kazi yake kubwa ni kuhakikisha wananchi wanalima zao hilo sambamba na kupata elimu ya kilimo cha pamba.

Naye Balozi wa Pamba Tanzania ndg, Agrey Mwanri amewataka wakazi wa Kibiti kuhakikisha kilimo cha pamba hakipotei tena Wilayani humo na kupitia zao hilo mapato yataongezeka kwa mkulima mmoja mmoja huku akisisitiza kuwa katika kipindi cha mauzo kila kilo moja itakayouzwa 3% itaingizwa kwenye mfumo wa Halmashauri.

Aidha mwekezaji wa zao la pamba Ndg. Soundar Velusamy ambaye ni kitukuu cha waliokuwa wanunuaji wakubwa wa Pamba ya Rufiji amesema ameamua kuja kuwekeza Kibiti na Rufiji kutokana na historia ya mababu zake, hivyo yuko tayari kushirikiana na wananchi kufufua kilimo cha zao hilo.

"Ukifuatilia historia, pamba ya Rufiji ndiyo pamba yenye ubora zaidi yenye nyuzi ndefu inavyotakiwa kwenye soko la Dunia" Alisema Velusamy.

Naye Diwani wa Maparoni Mhe. Bakari Mpate ambaye ni mbeba maono wa zao la pamba alisema, kipekee amefarijika sana Bodi ya pamba Rufiji kukubali kufufua Tena zao hilo. Zao hilo litaleta tija sana hususani katika mapato ya Halmashauri ya Kibiti.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.