• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KIKAO CHA LISHE ROBO YA PILI

Posted on: January 24th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Kibiti inafanya juhudi ili kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula shuleni  ikiwa  sehemu ya kumuunga mkono Raisi wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Mhe.Dr Samia Suluhu Hassan ambapo suala la lishe shuleni katika uongozi wa awamu ya 6 limekuwa kipaumbele kuhakikisha watoto wote wanapata chakula shuleni kwa siku zote za shule.

Hayo yamejiri katika kikao cha lishe kwa kipindi cha robo ya pili ambapo idara ya Elimu imetakiwa kuwa na mikakati ya kudumu ya kuhakikisha watoto wanapata chakula wanapokuwa shuleni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Afisa Utumishi Halima Ngota ameiagiza kamati ya lishe kuhakikisha mambo waliyokubaliana katika kikao hicho yanafanyiwa kazi ili kufikia malengo waliojiwekea.

Akiwakilisha taarifa ya lishe Afisa lishe wilaya ya kibiti Samson Minja amesema wanaendelea na juhudi za kuhakikisha lishe inapatikana katika shule zote ndani ya wilaya ya Kibiti na kuanzishwa kwa bustani. Vilevile amesisitiza uanzishwaji wa club za lishe kwenye shule ambapo mpaka sasa idara ya Lishe imeanzisha shamba darasa la karanga katika Hospitali ya wilaya lengo likiwa ni kutoa hamasa kwenye jamii kuona umuhimu wa uwepo wa Lishe.

Katika kikao hicho idara mbalimbali zimewasilisha taarifa ya hali ya lishe ambapo Afisa Taaluma Mariam msofe wa  elimu ya msingi amesema,mpaka sasa shule 48 kati ya 83 zinatoa chakula shuleni wanatarajia kufikia Februari 2023 kuweza kutoa huduma hiyo kwa shule zote huku akisema uhamasishaji unaendelea sambamba na kuwasihi wazazi kuchangia na shule zimeshaanza shughuli za kilimo cha matunda na mbogamboga kwa ajili ya kuboreshwa lishe.

Kwa upande wa elimu sekondari Afisa Elimu Anna Shitindi amebainisha kuwa mkakati wa idara yake mwaka huu ni kuhakikisha shule zote 15 za Sekondari zilizopo zinapata chakula.  Licha ya  kupatikana kwa chakula ameitaka  idara ya lishe na kilimo kupita shuleni kutoa elimu jambo ambalo litakuwa ni chachu ya kuona umuhimu uwepo wa chakula shuleni.

Vilevile idara ya kilimo na mifugo Kaimu Afisa kilimo shemwelwa Bandio na Afisa mifugo Suzan Kawiza wamesema suala la kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji  limetekelezwa kwa kutoa ushauri, elimu ikiiwa ni pamoja na kuwasisitiza kuhifadhi vyakula na kuweka akiba ya mifugo kwa matumizi ya  baadae, kulima mazao yanayostahimili ukame huku  akiahidi kuendelea kushirikiana na idara ya elimu sekondari na msingi kuendelea kutoa elimu ya lishe shuleni.

Aidha Afisa Maendeleo ya Jamii Hamis Mnubi  amesema idara yake imefanikiwa kutekeleza upatikanaji wa lishe kwenye Jamii kwa kutoa mikopo kwenye vikundi vya wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu .Alifafanua kuwa lengo la mkopo ni kuwawezesha kujiingizia kipato kupitia biashara ndogondogo na kuweza kurahisisha upatikanaji wa chakula na kuboresha chakula kwenye Jamii ambapo fedha hizo pia  hutegemea mzunguko kwa namna wanavyorejesha.

Mwisho Mganga Mkuu wa wilaya Daktari Elizabeth Oming'o ameipongeza idara ya elimu kuona umuhimu wa Maafisa lishe na kilimo kufika  na kutoa elimu ya lishe shuleni sambamba na kuanzishwa kwa bustani za mbogamboga n.k. Pia amesisitiza kuhakikisha shule zote watoto wanapewa chakula muda wa shule ili waweze kusoma bila ya kuwa na mawazo ya njaa darasani kwani lishe ni kipaumbele kwenye elimu kama Mhe.Rais alivyoelekeza. Pia ameitaka idara ya mifugo kuhamasisha wafugaji kuhakikisha watoto wanapata japo yai moja kwa mwezi Kwa ajili ya kujenga afya zao.

Matangazo

  • KUANZA KWA MFUMO MPYA WA UKUSANYAJI MAPATO (TAUSI) March 01, 2023
  • KUANZA KWA MFUMO MPYA WA UKUSANYAJI MAPATO (TAUSI) March 01, 2023
  • TANGAZO KWA WAFUGAJI WOTE WILAYA YA KIBITI December 29, 2022
  • TANGAZO KWA WAKULIMA WOTE WILAYA YA KIBITI December 30, 2022
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • WILAYA YA KIBITI YASHEHEREKEA MIAKA 106 YA SKAUTI NCHINI

    March 11, 2023
  • UKAGUZI WA UJENZI WA VYUMBA VITANO VYA MADARASA PAMOJA NA OFISI SAMBAMBA NA UKAGUZI WA KPI (KEY PERFORMANCE INDICATORS) SHULE YA MSINGI KIASI.

    March 09, 2023
  • SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAFANA WILAYANI KIBITI.

    March 07, 2023
  • MAAFISA UGANI NA WATENDAJI WA KATA WAKABIDHIWA PIKIPIKI-WIAYANI KIBITI.

    March 06, 2023
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.