• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KIKAO CHA LISHE ROBO YA PILI

Posted on: January 24th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Kibiti inafanya juhudi ili kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula shuleni  ikiwa  sehemu ya kumuunga mkono Raisi wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Mhe.Dr Samia Suluhu Hassan ambapo suala la lishe shuleni katika uongozi wa awamu ya 6 limekuwa kipaumbele kuhakikisha watoto wote wanapata chakula shuleni kwa siku zote za shule.

Hayo yamejiri katika kikao cha lishe kwa kipindi cha robo ya pili ambapo idara ya Elimu imetakiwa kuwa na mikakati ya kudumu ya kuhakikisha watoto wanapata chakula wanapokuwa shuleni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Afisa Utumishi Halima Ngota ameiagiza kamati ya lishe kuhakikisha mambo waliyokubaliana katika kikao hicho yanafanyiwa kazi ili kufikia malengo waliojiwekea.

Akiwakilisha taarifa ya lishe Afisa lishe wilaya ya kibiti Samson Minja amesema wanaendelea na juhudi za kuhakikisha lishe inapatikana katika shule zote ndani ya wilaya ya Kibiti na kuanzishwa kwa bustani. Vilevile amesisitiza uanzishwaji wa club za lishe kwenye shule ambapo mpaka sasa idara ya Lishe imeanzisha shamba darasa la karanga katika Hospitali ya wilaya lengo likiwa ni kutoa hamasa kwenye jamii kuona umuhimu wa uwepo wa Lishe.

Katika kikao hicho idara mbalimbali zimewasilisha taarifa ya hali ya lishe ambapo Afisa Taaluma Mariam msofe wa  elimu ya msingi amesema,mpaka sasa shule 48 kati ya 83 zinatoa chakula shuleni wanatarajia kufikia Februari 2023 kuweza kutoa huduma hiyo kwa shule zote huku akisema uhamasishaji unaendelea sambamba na kuwasihi wazazi kuchangia na shule zimeshaanza shughuli za kilimo cha matunda na mbogamboga kwa ajili ya kuboreshwa lishe.

Kwa upande wa elimu sekondari Afisa Elimu Anna Shitindi amebainisha kuwa mkakati wa idara yake mwaka huu ni kuhakikisha shule zote 15 za Sekondari zilizopo zinapata chakula.  Licha ya  kupatikana kwa chakula ameitaka  idara ya lishe na kilimo kupita shuleni kutoa elimu jambo ambalo litakuwa ni chachu ya kuona umuhimu uwepo wa chakula shuleni.

Vilevile idara ya kilimo na mifugo Kaimu Afisa kilimo shemwelwa Bandio na Afisa mifugo Suzan Kawiza wamesema suala la kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji  limetekelezwa kwa kutoa ushauri, elimu ikiiwa ni pamoja na kuwasisitiza kuhifadhi vyakula na kuweka akiba ya mifugo kwa matumizi ya  baadae, kulima mazao yanayostahimili ukame huku  akiahidi kuendelea kushirikiana na idara ya elimu sekondari na msingi kuendelea kutoa elimu ya lishe shuleni.

Aidha Afisa Maendeleo ya Jamii Hamis Mnubi  amesema idara yake imefanikiwa kutekeleza upatikanaji wa lishe kwenye Jamii kwa kutoa mikopo kwenye vikundi vya wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu .Alifafanua kuwa lengo la mkopo ni kuwawezesha kujiingizia kipato kupitia biashara ndogondogo na kuweza kurahisisha upatikanaji wa chakula na kuboresha chakula kwenye Jamii ambapo fedha hizo pia  hutegemea mzunguko kwa namna wanavyorejesha.

Mwisho Mganga Mkuu wa wilaya Daktari Elizabeth Oming'o ameipongeza idara ya elimu kuona umuhimu wa Maafisa lishe na kilimo kufika  na kutoa elimu ya lishe shuleni sambamba na kuanzishwa kwa bustani za mbogamboga n.k. Pia amesisitiza kuhakikisha shule zote watoto wanapewa chakula muda wa shule ili waweze kusoma bila ya kuwa na mawazo ya njaa darasani kwani lishe ni kipaumbele kwenye elimu kama Mhe.Rais alivyoelekeza. Pia ameitaka idara ya mifugo kuhamasisha wafugaji kuhakikisha watoto wanapata japo yai moja kwa mwezi Kwa ajili ya kujenga afya zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.