• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KIKAO CHA TATHIMINI YA MKATABA WA LISHE NGAZI YA KATA KWA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

Posted on: July 30th, 2024

Mwenyekiti wa Kamati ya tathmini ya mkataba wa lishe ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo ameongoza kikao na kupokea taarifa ya tathmini ya utekelezaji wa Mkataba ya lishe Wilaya ya Kibiti kwa ngazi ya Kata kwa robo ya nne (Aprili- Juni) ya mwaka wa fedha 2023/2024.

Akiwasilisha taarifa hiyo kwenye kikao hicho kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Julai 29, 2024 Afisa lishe Wilaya Bi. Roina Daza amesema kamati imefanikiwa kutekeleza shughuli nyingi kwa robo ya nne ikiwemo kuandaa mradi wa lishe kwaajili ya shughuli za mwenge wa uhuru, kufanya vikao vya WDC, kutekeleza kampeni ya ugawaji wa matone ya vitamini A kwa watoto, kutoa Elimu ya lishe, kupima pamoja na kutoa matibabu kwa watoto waliobainika kuwa na utapiamlo mkali.

Aidha Katibu tawala Wilaya ya Kibiti Bi. Maria Katemana ameipongeza kamati kwa jitihada kubwa za utekelezaji wa mkataba huo ikiwemo uwekaji wa taarifa za lishe kwenye mbao za matangazo za vijiji kwa 100% jambo ambalo halikuwa likifanyika hapo awali huku akisisitiza kushirikiana na idara ya kilimo kuhamasisha wakulima kupanda mbegu lishe kama vile mchicha lishe, maharage lishe, viazi lishe n.k.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, Ndg. Hemed Magaro amesema tayari amewapatia maelekezo idara ya Kilimo, mifugo na uvuvi kwenye kikao cha lishe cha wataalamu kuhakikisha kuwa wanatoa msaada wa kitaalamu na kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara hususani kwenye ngazi ya shule.

“Tumewaagiza wenzetu wa kilimo wahakikishe wanatoa msaada wa kitaalamu, ushauri na kusimamia wakulima kule vijijini bila kusahau shule zetu ili kila shule iwe na bustani za mbogamboga lakini pia kupeleka miche ya mikorosho kwenye shule zenye mashamba makubwa kama Kibiti Sekondari ili mashamba hayo yalete tija” Alisema Magaro.

Akifunga kikao hicho Kanali Kolombo amekitaka kitengo cha lishe kuendelea kuwapatia huduma watoto 71 waliobainika kuwa na udumavu, kufanyia kazi ushauri wa wajumbe wa kuanzisha utaratibu wa kupima hali za lishe za watumishi wa Kibiti ikibidi kuwa na wiki ya lishe Wilaya ili kutoa huduma hizo pamoja na kuwapa elimu wananchi juu ya uongezwaji wa virutubishi kwenye vyakula vyao kama vile unga, mafuta n.k.

Pia Kanali Kolombo amewataka watendaji kutodharau jitihada zao kwani malengo ya kata yakifikiwa ndivyo Halmashauri, Mkoa na Taifa litakavyofikia malengo yake.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.