• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

Posted on: December 9th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti imeungana na watanzania wote nchini kusheherekea miaka 61 ya Uhuru wa  Tanzania bara  katika ukumbi wa Ofisi za Halmashauri ambayo nchi nzima yamefanyika katika ngazi ya Wilaya na kusheheneshwa na kauli mbiu ya mwaka isemayo AMANI NA UMOJA NI NGUZO YA MAENDELEO YETU.

Kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya Wilaya  Mohamed Mavura, amewapongeza wananchi na watumishi wa ngazi mbalimbali chama na Serikali na viongozi wa dini kwa namna walivyojitokeza kuitikia wito wa kusheherekea miaka 61 Tanzania . Aidha Bwana Mavura ameeleza jinsi ambavyo Serikali imefanya kazi kubwa kwa Halmashauri yetu, ikiwa ni Pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo iliyokamilika na inayoendelea kujengwa katika kada mbalimbali hususani, Elimu, Afya, Miundombinu ya barabara, maji, umeme n.k

Akizungumzia kwa niaba ya Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Meja Edward Gowele ambaye alikuwa mgeni rasmi, Katibu Tawala wa wilaya (DAS) Ndg. Milongo Sanga  amesema tangu kupata uhuru kibiti inajivunia kwa kuwa na mafanikio yenye tija katika sekta  mbalimbali za kilimo ,viwanda,Elimu,miundo mbinu Afya maji n.k jambo ambalo awali haikuwa rahisi katika maeneo yetu ya kibiti.

Vile vile Sanga amesema Pato la wilaya limeongezeka mara dufu Kutoka Tsh.939,791,435.20 kwa mwaka 2016-17 Hadi kufikia TSH.2,492,877,687.49 kwa mwaka 2021-22 hayo ni mafanikio makubwa ambayo kibiti inajivunia kuyapata ndani ya miaka 61 ya uhuru na tangu kuanzishwa kwa Wilaya ya Kibiti.

Hata hivyo maadhimisho hayo yaliambatana na utoaji wa zawadi ya cheti na fedha taslimu kwa washindi wa uandishi wa Insha kutoka shule za msingi na sekondari ulioanza kushindanishwa tangu tarehe 1/12/2022 kabla ya kilele cha maadhimisho kama ilivyoekezwa na Serikali.

Maadhimisho yaliambatana na watoa mada 6 ambao Kwa nyakati tofauti wameipongeza Serikali Kwa namna inavyohakikisha Tanzania inapata Maendeleo ukilinganisha na kipindi cha nyuma hususani katika Wilaya ya kibiti mafanikio yameonekana katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu Elimu Afya n.k. bila kusahau uzalendo ambao ni nguzo ya ujenzi wa Taifa .

Vilevile Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Ramadhani Mpendu akizungumza katika sherehe hiyo amewapongeza washiriki wote wa sherehe hiyo wakiwemo watoa mada mbalimbali, viongozi wa Dini na washiriki wote kwa ujumla pia  amewataka wakazi wa kibiti na watumishi kwa ujumla kufanya kazi Kwa bidii ili kuendeleza mafanikio yaliyopatikana kwani kibiti kwa Maendeleo inawezekana .

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.