• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MAADHIMISHO YA SIKU YA MIKOKO DUNIANI YAFANA WILAYANI KIBITI.

Posted on: July 26th, 2023

Kwa mara ya kwanza, siku ya mikoko duniani Tanzania imeadhimishwa katika Wilaya ya kibiti katika uwanja wa shule ya Sekondari ya  Wavulana Kibiti na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali ambapo shirika la WWF limewezesha kufanyika kwa sherehe hizo.

Lengo la kusheherekea siku hiyo ya mikoko duniani ni kuikumbusha Jamii ya mwambao wa Pwani na na Jamii inayotegemea mazingira ya Pwani, kushirikiana na Serikali, taasisi za mashirika mbalimbali mpaka ngazi ya Taifa kuhifadhi Misitu ya mikoko katika nchi ya Tanzania yenye ukubwa wa hekari 158,000 sawa na 0.4% ya eneo lote la Misitu Tanzania bara hekari mil.48.1.

" Tarehe 26.7. Kila mwaka  ilipitishwa kipekee iwe siku ya kusheherekea  mikoko ukilinganisha na misitu yote "Alisema Modesta Meddard Msimamizi wa miradi ya Pwani na Bahari

" Tunamshukuru WWF kwa kuona umuhimu na kuchukua fursa ya kikanuni na kisheria kuadhimisha siku ya mikoko kikanda katika wilaya ya Kibiti " Alisema  Modesta.

Akizungumzia faida za misitu ya mikoko Bi. Modesta  amesema, mikoko ina uwezo wa kupunguza gesi joto(carbon) mara 10 zaidi ya misitu yote na kupunguza hewa ya carbon mara 5 zaidi ya misitu yote mikubwa barani Afrika .

Licha ya eneo la misitu ya mikoko kuwa dogo bado Ina uwezo mkubwa wa kuuza gesi joto aina ya carbon mara 4 zaidi ya misitu mikubwa duniani kama vile misitu ya Amazon

Hata hivyo aliendelea kusema kwamba  mikoko huchangia kwa 75% kutengeneza mazalia ya samaki, kuzuia mmomonyoko wa udongo (ardhi) n.k.

Aidha Msimamizi wamiradi kanda ya  Pwani na bahari Tanzania amelishukuru shirika la WWF kwa kushirikiana na wanakibiti kwa mara ya kwanza kusheherekea siku hii muhimu ambapo awali walikuwa wakiadhimisha katika Wilaya ya mafia.

" Kusheherekea maadhimisho haya kibiti kutaleta mwamko na shamrashamra kwani wazawa watapata uelewa zaidi wa usimamizi wa mikoko"Alisema Frank Sima (Afisa Mhifadhi Mkuu TFS).

Bw. Sima ameeleza kuwa Moja ya shughuli wanazozifanya ni utunzaji wa mazingira na kuisaidia jamii kujikwamua kiuchumi Kwa kufanya shughuli mbalimbali kupitia vikundi takribani 502 na BMU 271 katika vijiji vya za kibiti.

Vilevile Sima aliongeza kuwa, kiutendaji wanafanya kazi na wilaya 6 kikanda ambazo ni ambazo ni Wilaya ya Kibiti, Mafia, Mkuranga, Rufiji, Kilwa na kigamboni (DSM).

Kipekee Bi. Modesta amesisitiza suala la ushirikiano ili kuweza kuhifadhi Misitu huku akiwapongeza wakala wa huduma za misitu Tanzania TFS kwa kazi nzuri wanazofanya kuhakikisha Uhifadhi unadumu

"Tusipotunza mazingira, tutapoteza samaki waishio baharini na maisha ya  wengi wanaotegemea bahari yatakuwa hatarini"Alisema Zakayo Mlenduka mgeni rasmi wa shughuli hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya KIbiti.

Ikumbukwe kuwa, kati ya aina 7 ya mikoko inayopatikana duniani, aina 6 hupatikana katika delta ya Rufiji Wilaya ya Kibiti.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.