• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

Maadhimisho ya Siku ya Wavuvi ki Wilaya yafanyika Pombwe kata ya Kiongoroni

Posted on: November 21st, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti na Tanzania kwa ujumla imeungana na nchi  nyingine ulimwenguni kuazimisha siku ya uvuvi Duniani yenye kauli mbiu ya Bahari ni kioo chetu , katika kijiji cha Pombwe kata ya Ruma  Tarafa ya Mbwera wilayani humo.

Maadhimisho hayo huadhimishwa Kila mwaka ifikapo Novemba 21 kwa lengo la kuwakumbusha wavuvi,  namna sahihi ya kuzingatia taratibu na Sheria za uvuvi hususani katika zana za kuvulia, kuchukua tahadhali wanapokua katika kazi za uvuvi baharini pia kutengeneza umoja wa wavuvi ili kwa Pamoja waweze kutatua changamoto zinazowakabili na kuelekezana njia sahihi za uvuvi.

Hayo yamebainishwa na Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Kibiti Japhet Manyama alipokuwa akitoa ufafanuzi wa maadhimisho hayo wakati akimkaribisha mgeni rasmi kwenye hafla hiyo kuzungumza na wananchi wa  Kijiji cha pombwe.

Akizungumza AfisaTarafa ya Mbwera Lucas Magai kwa niaba ya mkuu wa Wilaya ya Kibiti Meja Edward Gowele ambaye alikua mgeni rasmi katika hafla hiyo, amewapongeza wakazi wa Kijiji hicho kwa namna walivyojitokeza katika maadhimisho hayo na amewasisitiza  wakazi hao kushirikiana na BMU kuhakikisha hali ya usalama inakua shwari katika Kijiji cha pombwe huku akiwataka wakazi hao kutoa taarifa za wageni wanaoingia na kutoka katika kisiwa hicho. Pia Magai amependekeza kuanzishwa kwa mafunzo ya mgambo kwa vijana wanaotoka  katika jamii inayoishi  delta ili kuimarisha hali ya usalama kwa muda wote visiwani .

Vilevile Magai amewataka wakazi hao kuchukua tahadhari juu ya magonjwa mbalimbali kama vile UKIMWI na CORONA kutokana na mwingiliano wa watu, kwani hivi karibuni nchini china kumetokea vifo vya watu takribani 6 waliopoteza maisha kwa  ugonjwa wa corona jambo ambalo wengi huamini kuwa ugonjwa huo umekwisha kutoweka.

Afisa Tarafa Magai amekemea suala la utoro mashuleni katika maeneo ya uvuvi na kuwataka wazazi kutekeleza majukumu yao kwa kusimamia na kuhakikisha watoto wanakwenda shule sambamba kuwapa mahitaji, Pia amesema kuwa Serikali imesimamia elimu bila malipo darasa la kwanza mpaka kidato cha 6 Ili kuhakikisha Kila mtoto anapata elimu.

Pamoja na hayo Bw. Magai amewaagiza wakazi wote wa delta ikiwa ni pamoja na kina Mama kuunda vikundi vitakavyowasaidia kupata mikopo ya kufanyia biashara mbalimbali ili kuweza kjikwamua kimaisha na kuwasihi wavuvi kuwekeza fedha wanazozipata kwa manufaa ya baadae.

Aidha sherehe hiyo ilitumbuizwa kwa michezo mbalimbali kama vile kuvuta kamba kukimbia, kuogelea, kuvusha mitumbwi, maigizo na mashairi yaliyosheheni vina vyenye maudhui ya matumizi sahihi ya Bahari na rasilimali zake sambamba na zoezi la kutoa zawadi kwa Washiriki wa michezo hiyo.

Mwisho Magai ameahidi kuzibeba changamoto zilizopo kijijiji hapo kwa kuzifikisha katika ngazi husika hususani kupata muafaka wa uhakika wa mmiliki halali wa kisiwa cha Simaya kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti na kilwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.