• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MAAFALI YA 23 YA KIDATO CHA SITA YA KIBITI SEKONDARI.

Posted on: February 23rd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amewataka wazazi , walimu na bodi ya shule kusimamia maadili ya watoto katika mazingira wanayoishi kuhakikisha  wanawajengea nidhamu itakayowawezesha kuishi na jamii vema wakiwa shuleni na baada ya kumaliza shule.

“malezi ya watoto ni jukumu letu sote,tushirikiane kufuatilia maadili ya watoto  hasa huko mabwenini wanakolala na wanapokuwa majumbani” alisema Kolombo.

Amesema hayo katika mahafali ya 23 ya shule ya Sekondari ya wavulana kibiti ambapo alikuwa ndiye   Mgeni rasmi pia ametoa pongezi kwa Mhe. Rais Dr.Samia Suluhu kwa kuwekeza fedha nyingi katika idara ya elimu.  Sambamba na hilo amepongeza  jitihada zote  na Walimu,wazazi na walezi   kuhakikisha ufaulu unaongezeka shuleni bila kujali changamoto zinazojitokeza kwa kujitoa kuunga mkono jitihada zinazofanywa shuleni hapo kwa hali na mali.

“Jitihada zenu zimeleta ufaulu mzuri, endeleeni na utaratibu huu tuweze kutokomeza zero kibiti” alisema Kanali Kolombo.

Akijibu changamoto zilizoainishwa katika risala ya  Mkuu wa shule ,wanafunzi wanaomaliza na wanaobaki Kanali Kolombo  amesema amezibeba na ameahidi kuzifanyia kazi kwa kushirisha na Halmashauri au taasisi nyingine ili kuweza kutatua changamoto hizo.

Aidha akiwa shuleni hapo Kanali Kolombo ameahidi kuchangia sh 500,000 kwa ajili ya kuendeleza mradi wa kutengeza  sabuni unaofanywa na klabu ya wanafunzi wajasiliamali shuleni hapo, pia ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi 300,000 kwa ajili ya kuunga Mkono jitihada za wazazi katika kuunga Mkono shughuli za Kitaaluma shuleni hapo.

Kwa nyakati tofauti wakisoma risala ya wanafunzi pamoja na taarifa ya Mkuu wa shule wamesema,  shule imekuwa na mafanikio mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupandisha ufalu wa wanafunzi kwa miaka sita mfululizo licha ya kuwa bado wanakabiliwa na changamoto kadha wa kadha  kama vile uvamizi wa eneo la shule, kukosa mfumo wa kisasa wa gesi ya kupikia chakula cha wanafunzi, upungufu wa samani na ukosefu wa usafiri wa shule  kwa muda mrefu, upungufu wa vitabu vya kiada na ziada, na upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi na Hesabu.

Katika hatua nyingine Katibu wa jumuiya ya wazazi shuleni hapo Mhandisi Kaiza John ameendesha Harambe na kupata zaidi  ya sh. milioni moja lengo likiwa ni kusaidia  kukwamua changamoto za shule ikiwa ni pamoja na kulipa mshahara wa walimu watatu wanajitolea kufundisha shuleni hapo kutokana na upungufubwa walimu pia wanatarajia  kununua mashine ya kudurufu (photocopy mashine).

Naye Meneja mahusiano wa huduma za wateja wa Azania Bank ndg. Othman Jebra (mwanamfunzi wa Kibiti sekondari miaka ya nyuma ) akiwa ameambatana na Afisa mahusiano  wa Bank hiyo Bakari Mmbaga wametoa zawadi kwa washindi  wa 3 waliofanya vizuri zaidi katika mitihani yao, ambapo mshindi wa kwanza amepata sh150,000, mshindi wa pili amepata sh 100,000 na mshindi wa tatu amepata sh 70,000. Jebra amesema wametoa zawadi ili kutoa hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii na kurudisha shukrani kwenye jamii hususaani katika shule aliyosoma miaka kadhaa iliyopita huku akiwataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili waweze kufanya vizuri mitihani yao ya kumaliza kidato cha 6.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.