• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MIAKA 62 YA UHURU WA TANZANIA BARA WILAYANI KIBITI

Posted on: December 12th, 2023

WAZEE WATHIBITISHA UWEPO WA MAENDELEO NDANI YA MIAKA 62 YA UHURU.

9.12.2023.

Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti imeungana na Wilaya nyingine zote nchini kusheherekea maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania bara.

Sherehe hizo zimefanyika kwenye kila Wilaya nchini ikiwa ni maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. SSH  aliyeagiza sherehe hizo kufanyika kwa kufanya shughuli za kijamii, mijadala na uandaaji wa dira ya Taifa 2025  - 2050.

Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, shughuli za kijamii zilizofanyika ni: kufanya usafi katika eneo la soko la Kibiti kisha kufuatiwa na mchezo wa kirafiki wa mpira wa miguu kati  ya timu ya KURUGENZI FC na KIBITI UNITED uliofanyika katika Uwanja wa Samora – Kibiti, ambapo timu hizo zilitoka sare ya goli 1-1, mambo haya yalifanyika siku moja kabla ya maadhimisho yaani tarehe 08-12-2023.

Pia kulifanyika Mashindano ya insha na utunzi wa ushairi mashuleni wiki moja kabla ya sherehe hizo na washindi wote walikabidhiwa zawadi tarehe 09-12-2023, siku ya maadhimisho hayo ambayo yalifanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri. Sambamba na hilo siku hiyo pia ulifanyika mdahalo uliowashirikisha WAZEE MAARUFU ambao waliweza kuelezea kinagaubaga maendeleo yaliyofikiwa ndani ya Wilaya kwa kipindi cha miaka 62 ya UHURU.

Akichokoza mada kabla ya mdahalo kuanza, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bw. Hemed Magaro alichagiza kwa kuelezea maendeleo yaliyopatikana katika miaka 62 ya UHURU ndani ya Wilaya hivyo kuonesha namna ambavyo Kibiti imepiga hatua kubwa kimaendeleo.

Magaro amesema Licha ya Halmashauri kuwa changa mpaka sasa kuna ongezeko kubwa la shule za Msingi na Sekondari,vituo vya Afya, zahanati ongezeko la chakula katika Sekta  ya Kilimo na pato la Wilaya limeongezeka .

Aliendelea kusema kuwa pato la Wilaya limeongezeka kutoka makusanyo ya 9,390,000 mpaka  kufikia Bil 1.18 na tunatarajia kukusanya takribani bil 2 na point kadhaa kwa mwaka huu, haya ni maendeleo makubwa.

Vilevile Mhandisi Ayubu Ngereza amesema kwa upande Barabara ,maji na umeme Wilaya imepiga hatua kubwa ambapo mpaka sasa Barabara nyingi zinapitika na maeneo mengi kufikika, mpaka sasa 68.4% ya wakazi wa Vijijini na 67% ya wakazi wa mjini wanapata maji kutoka vyanzo mbalimbali vya maji ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Aidha wazee wa zamani wa Kibiti walioshiriki mdahalo kwa nyakati tofauti, wameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana nchini kwani kila mwenye macho anaona haambiwi tazama.

Katika awamu zote za uongozi tumepiga hatua, Sasa tuna shule nyingi, vituo vya Afya, zahanati, Barabara zinaendelea kujengwa na zinapitika, huduma za maji na umeme  zinapatikana pamoja na kwamba bado kuna changamoto .

Wazee hao kwa umoja wao wamewataka viongozi wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia vizuri kila kitu kilichopo ili kuleta maendeleo zaidi, huku wakiwataka kufufua mambo mengine ambayo hayakuwezekana katika kipindi cha miaka ya nyuma, kama vile kilimo cha zao la pamba ambalo ndilo  lilikuwa zao la biashara Wilayani Kibiti kabla ya kushamiri kwa mazao ya korosho na ufuta.

"Katika maadhimisho haya tulipewa maelekezo na  Mhe. Rais tumetekeleza kwa kufanya yote tuliyoagizwa ikiwa ni pamoja na kuandaa mdahalo huu kujadili mafanikio yaliyofikiwa katika wilaya yetu" Alisema Kolombo.

"Kama mlivyosikia katika mdahalo, wazee wamekiri kuwepo kwa maendeleo makubwa katika nyanja mbalimbali za mahitaji muhimu ya kila siku ikiwemo miundombinu yote kama vile Elimu, Afya , Maji, Barababa, Umeme, Kilimo, Ongezeko la pato la wilaya n.k.

Kanali Kolombo amesema Serikali inaendelea kufanya jitihada kubwa kuhakikisha maendeleo yanapatikana ndiyo maana inaendelea kuleta fedha mbalimbali za kutekeleza miradi katika wilaya yetu.

"Nimesikiliza mdahalo kwa makini wazee wangu nimewasikia mawazo, maoni , ushauri nimeyabeba na Serikali yetu ni sikivu, ninaimani yote mliyowasilisha leo yatatekelezwa" Alisema Kolombo.

Vilevile Kanali Kolombo kupitia kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya Uhuru mwaka 2023 isemayo MIAKA 62 YA UHURU, "UMOJA NA MSHIKAMANO NI CHACHU YA MAENDELEO YA TAIFA LETU" amewataka Wana kibiti kuhakikisha wanakuwa na UMOJA na MSHIKAMANO kuhakikisha Kibiti inasonga mbele.

Akihitimisha maadhimisho hayo, Kanali Kolombo amewataka wazazi na walezi katika kipindi hiki cha likizo kuhakikisha wanawaandikisha shule watoto wote wenye umri wa kuanza darasa la Awali na Msingi katika shule mbalimbali zilizopo hapa Wilayani kwani kupata Elimu ni haki ya kila Mtanzania.

"Ndugu zangu ni wakati wa likizo hakikisheni watoto wenye umri kati ya miaka 4-6 wanaandikishwa madarasa ya Awali na Msingi na wale darasa la saba waliofaulu wanapelekwa shule za sekondari kama watakavyopangiwa, kwa yeyote ambaye hatofanya hivyo hatua za kisheria ziitachukuliwa" alisema Kolombo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.