• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MKURUGENZI MAGARO ATETA NA WASAIDIZI WAKE.

Posted on: July 25th, 2023

ASISITIZA UKUSANYAJI NA USOMAJI WA MAPATO NA MATUMIZI.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Bw. Hemed Magaro, kwa mara ya kwanza amekutana na watendaji wa Kata, Watendaji wa Vijiji, Makatibu Tarafa na Wakuu wa Wakuu wa shule za msingi na sekondari, na Wakuu wa Idara katika kikao kazi ili kupeana dira na kupanga mikakati ya pamoja kwa maendeleo ya kibiti.

Katika kikao kazi hicho ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, Bw. Magaro amewaagiza watendaji wa Vijiji na Kata, kukusanya na kusimamia mapato kikamilifu, ikiwa ni pamoja na  kuwasomea wananchi taarifa ya mapato na matumizi na kuyabandika kwenye mbao za matangazo kila baada ya miezi mitatu.

" Kuwe na uwazi, kusanyeni mapato na wasomeeni wananchi mapato na  matumizi ili waweze kujua fedha za serikali zilizoingia, mapato yaliyokusanywa pamoja na matumizi yake" Alisema Magaro.

Vilevile Mkurugenzi Magaro ameagiza taarifa ya mapato na matumizi kusomwa kila baada ya miezi mitatu yaani  kabla ya tarehe 10 ya mwezi unaofuata, sambamba na kuhakikisha kila Kijiji kina account ya Benki ambayo itatumika kuhifadhi fedha zinazokusanywa.

" Watendaji Kata nasisitiza, taarifa ya makusanyo ya mapato ikawe kipaumbele katika mabaraza yenu ya Kata " Alisema Hemed Magaro.

Hata hivyo katika kikao hicho Bw. Magaro amewaagiza Wakuu wa shule, Walimu wa kuu na waratibu wa Elimu Kata kukagua, kusimamia na kudhibiti utoro na mimba shuleni kwani ni chanzo cha kushuka kwa ufaulu katika Wilaya ya Kibiti, ikiwa ni pamoja na kuunda timu ya kiutendaji  na kuwapa motisha hususani Walimu wao wanapofanya vizuri.

" Kuweni na mikakati, tafuteni mbinu mbalimbali za ufundishaji zitakazosaidia kupandisha ufaulu kwa wanafunzi" Alisema Bw. Magaro.

Katika kikao hicho Mkurugenzi ameelekeza wasaidizi wake wote aliokutana nao leo, kuhakikisha chakula kinapatikana mashuleni kwa kuwaelimisha wazazi kuona umuhimu huo, kwani chakula kikipatikana kitaleta utulivu kwa wanafunzi na kupandisha ufaulu kwa wanafunzi.

"Suala la upatikanaji wa chakula mashuleni siyo la Walimu pekee ni letu sote tushirikiane, ndiyo maana nimewakutanisha wote hapa”. Alisema Magaro.

Aidha Watendaji Kata na vijiji wametakiwa kuhamasisha kilimo ambacho ni UTI wa mgongo wa mapato  ya Wilaya kupitia Kata zao, pia Maafisa maendeleo Kata kusimamia vikundi vinavyokopeshwa na kuhakikisha wanarejesha na kuhamasisha jamii kushiriki katika miradi ya Maendeleo.

Mbali na hayo Mkurugenzi amemuagiza Afisa Utumishi kusimamia  watendaji wa Kata na Vijiji kutengeneza mpango kazi wa kila mwezi, miezi 3 , 6  mpaka  mwaka ambapo kila baada ya mwezi watendaji hao watasoma taarifa ya utekelezaji  utakaoonyesha  namna anavyotimiza majukumu yake kwa kusimamia nidhamu (kuheshimiana) kulingana na mipaka ya kazi.

Magaro amekemea pia tabia ya uuzaji holela wa ardhi kwa baadhi ya Watendaji wa Kata na Vijiji huku akiwasisitiza kujipanga vizuri  kwenda kusimamia vema uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambao unatarajiwa kufanyika mwakani ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwaka wa uchaguzi 2025.

"Swala la Uchaguzi ni sehemu ya kujitathmini kiutendaji kwa kutatua kero za wananchi katika maeneo yenu na kujenga mazingira mazuri ya kukubalika" Alisema Magaro.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.