• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MNADA WA MWISHO WA KOROSHO WAFANYIKA MKURANGA

Posted on: December 27th, 2023

20.12.2023.

Mnada wa Tano na wa mwisho katika msimu wa korosho mwaka 2023 Mkoa wa Pwani umefanyika leo Wilayani Mkuranga ukiwa na wazabuni watano na kufanikiwa kuuza jumla ya Tani 150,938.

Katika mnada huo korosho za daraja la kwanza zimeuzwa kwa sh 1415 na za daraja la pili kwa sh 1110 baada ya wakulima wote kukubaliana kuuza.

Akizungumza na wakulima waliohudhuria mnada huo, Meneja wa Bodi ya korosho Tawi la Dar re Salaam  Bi. Domina Mkangara amesema katika msimu huu changamoto ya hali ya hewa ( mvua) imesababisha kushuka kwa makusanyo ya korosho tofauti na matarajio waliyokuwa wamejiwekea.

"Tulitarajia kuuza Tani 20000, lakini tumeuza Tani 10500 hii yote ni kwasababu makusanyo yakorosho kushuka kutokana na changamoto ya hali ya hewa na kusababisha korosho nyingi kuwa chini ya kiwango". Alisema Bi Domina.

Kwa upande wa korosho zilizokuwa chini ya daraja la pili (reject ) wameweka utaratibu wa kuziuza katika soko la ndani kwa wabanguaji wa ndani kupitia vyama vyao vya ushirika.

"Wabanguaji wa ndani, hii ni fursa kwenu itumieni vizuri, hali ya upatikanaji wa  malighafi katika viwanda vyenu ipo wazi." Alisema Bi. Domina.


Vilevile kupitia soko hilo la ndani amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanapeleka korosho hizo kwenye AMCOS zao wakati utaratibu wa kuziuza ukipangwa na kudai kwamba watapewa utaratibu wakati wote kuanzia sasa. Pia amewasisitiza wakulima wote kuendelea  kuandaa mashamba kwa ajili ya msimu ujao sambamba na kulima mazao mengine katika kipindi hiki cha mvua.

Aidha Meneja wa Corecu Bw.Hamis Mantawela amesema mpaka wanafika mnada wa mwisho wa msimu wa korosho tayari Shilingi Bilion 20 zimetolewa kwa ajili ya malipo ya wakulima ambao mizigo yao ilipitia CORECU na hakuna anayedai.

Mbali na malipo Mantawela amewataka viongozi wa AMCOS kuruhusu usajili mpya kwa kupokea wanachama na  tayari Ofisi ya Mrajisi na Vyama vya Ushirika zinaandaa utaratibu wa kusajili wanachama wapya.


Pia Mantawela amevielekeza vyama vyote vya Msingi kutunza pembejeo zilizosalia kwa ajili ya matumizi  ya msimu ujao na kwa yeyote atakayekwenda kinyume na maelekezo hayo Sheria itachukua mkondo wake.

"Pembejeo zote ziko kwenye mfumo, na kila kinachotoka mfumo unaonyesha, chondechonde zitunzeni ni Mali ya Serikali.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya korosho Juma Abdallah Kibanyula amewashukuru wakulima wote  kuwa na uvumilivu mkubwa katika msimu huu ambao umesuasua kutokana na hali ya mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Mwisho Wakulima wameishukuru Bodi ya korosho kwa kuwasimamia vizuri ikiwa ni pamoja na usimamizi wa kuanika, kuhifadhi na kuhakikisha korosho zinauzika hasa katika msimu huu ambao umekuwa mgumu kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

"Tunawashukuru CORECU, kwa kutusimamia na kutuelekeza wakati wote, kutokana na hali ya hewa hatukutegemea kabisa kuuza korosho zetu, kipindi kilikuwa kigumu, cha kufukuzana na jua na mvua. Kazi ilikuwa ni kuanika na kuanua korosho." Walisema Wakulima.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.