• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

NDARUKE AMALIZA KERO YA VIONGOZI WA KIJIJI CHA NYANJATI WILAYANI KIBITI, AWAHAKIKISHIA MABOMA NYANJATI YANAKWENDA KUKAMILIKA. DC AHAIDI MABATI 80 KWA AJILI YA KUEZEKA.

Posted on: January 31st, 2024

Mwenyekiti  wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kibiti Mhe. Juma Ndaruke amefika katika kijiji cha Nyanjati kilichopo Kata ya Mahege ili kusikiliza na kutatua kero za viongozi wa kijiji hicho ambao walisusia shughuli za uongozi kijijini hapo kwa madai ya kuwa nafasi zao za uongozi zimewekwa rehani kwasababu ya kutokukamilika kwa maboma matatu yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi.

Viongozi hao walidai kuwa kutokamilika kwa maboma hayo ya muda mrefu kunakwamisha shughuli za maendeleo na pia kupoteza sifa zao za uongozi kwa Wananchi kijijini hapo.

Baada ya kusikiliza madai hayo Mh. Ndaruke amewahakikishia viongozi hao kuwa maboma hayo yatakamilika, kuonyesha kuwa anamaanisha hapohapo amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Mh. Kanali Joseph Kolombo kuongea na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Ndg. Hemed Magaro kukamilisha maboma hayo matatu haraka iwezekanavyo.

"Mkuu wa Wilaya ni wakati wa wewe kujadiliana na Mkurugenzi kuhakikisha angalau boma moja linakamilika kwa namna yeyote wakati tunasubiri fedha za umaliziaji, Serikali kupitia Halmashauri inawajibu wa kuwaunga mkono wananchi katika ukamilishaji wa maboma hayo" Alisema Mhe. Ndaruke.

Vilevile Mhe. Ndaruke amewapongeza wajumbe wa Kamati ya Kijiji hicho kwa kuwa na usimamizi mzuri wa kujenga majengo imara kwa kutumia nguvu  za wananchi.

Akipokea maelekezo hayo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema maelekezo ameyapokea na habari njema ni kwamba, tayari bati 80 zimekwishapatikana kwa ajili ya ukamilishaji wa boma moja kati ya maboma matatu na boma la utawala tayari limeshaingizwa kwenye bajeti.

"Ndg wajumbe naomba muwe na uvumilivu tupo kwenye utaratibu mzuri wa kuhakikisha maboma haya yanakamilika na ndani ya siku tatu kuanzia leo bati 80 zitakabdhiwa hapa kwa ajili ya kuezeka boma moja" Alisema Kolombo

Naye Katibu wa ccm Wilaya ya Kibiti Ndg Zacharia Muhidini amewasisitiza wajumbe wa Kijiji kukabiliana na changamoto zinazowakabili kwa kuhakikisha mwarobaini wa changamoto hizo unapatikana na siyo kuzikimbia changamoto kwa kutaka kujitoa katika nafasi zao.

Vilevile Katibu Muhidini ameiomba Serikali kuhakikisha umaliziaji wa maboma hayo unakamilika kabla ya uchaguzi kuanza  huku akisisitiza mazingira ya majengo hayo kusafishwa na kuwa safi wakati wote.


Hata hivyo,  Diwani wa Kata ya mahenge Mohamed Hingi amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuwa na mwitikio wa haraka baada ya kupewa taarifa ya wajumbe hao na kutoa maelekezo yenye faraja.

Awali wajumbe hao waligoma kuendelea kushiriki vikao vya aina yeyote kijijini hapo mpaka wajue hatma ya ukamilishaji wa maboma hayo kwani yanafanya waonekane wababaishaji kwenye jamii.

Mwisho Mtendaji wa Kijiji, Mwenyekiti wa Kijiji na baadhi ya wajumbe hao wamewashukuru viongozi hao kwa kufika huku wakisisitiza ahadi zilizowekwa zikamilike kwa vitendo na si maneno.


Hayo yote yamejiri tarehe 29.01.2024 katika kikao na wajumbe wa Kijiji hicho. 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.