• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

RC KUNENGE ATEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI WA TAMISEMI, ASISITIZA KUONGEZA KASI KWENYE UKUSANYAJI WA MAPATO.

Posted on: February 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amewaelekeza wajumbe wa Timu za Menejimenti (CMT) za Halmashauri ya wilaya ya Kibiti na Rufiji kuongeza jitihada za utekelezaji majukumu kwa kufanya kazi kwa bidii  ili waweze kuleta matokeo yatakayoweza kufikia malengo yaliyokusudiwa.

"Kila mtu atekeleze majukumu yake, tunatakiwa tukusanye mapato mengi zaidi kutoka kwenye vyanzo vyetu ili tuweze kutoa huduma kwa wananchi, na hilo linawezekana tukiweka malengo yetu vizuri” Alisema Kunenge.

Mhe. Kunenge amezisisitiza timu za Menejimenti za Halmashauri kusimamia ukusanyaji wa mapato kwa jitihada kubwa na kudhibiti mianya ya upotevu  wa mapato ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Maelekezo haya ni sehemu ya kazi zenu za kila siku, muwe na takwimu na mikakati madhubuti ya utendaji kwani maagizo hayo yanatarajia utendaji wa taaluma zenu ( wataalam) kwa kujituma zaidi.

Hayo yamejiri jana tarehe 14.2.2024 ikiwa ni sehemu ya  utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Mohamed  Mchengerwa ambapo aliwataka Wakuu wa Mikoa katika maeneo yao kukutana na timu za menejimenti za Halmashauri zao.

Maagizo ya Waziri wa TAMISEMI yameelekeza Wakuu wa Mikoa kufuatilia hali ya vipaumbele katika wakati huu wa maandalizi ya Mpango na bajeti ya Mwaka 2024/2025 vinavyojibu hoja za wananchi, mikakati ya ukusanyaji mapato na udhibiti wa mianya ya upotevu wa mapato hayo.


Maagizo mengine yameelekeza halmashauri kutoa taarifa zao za upelekaji fedha zitokanazo na mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo, ili usimamizi miradi hiyo ukamilike kwa wakati na kwa kiwango kinachoendana na kiasi cha fedha kilichotolewa, taarifa ya utoaji wa asilimia 10 za mapato ya ndani kwa vijana, wanawake na wenye ulemavu pamoja na mikakati ya utekelezaji taarifa za hoja za Mdhibiti na Mkagunzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG), za Kamati ya Bunge LAAC na (TAMISEMI).

Aidha wa Wakuu wa Wilaya za kibiti na Rufiji , Mhe. Kanali Joseph Kolombo na Meja Edward Gowele kwa nyakati tofauti walisema wamepokea maagizo yote na kuahidi kuyafanyia kazi kama walivyoelekezwa. Pia Wakuu hao wa Wilaya wamesema hali ya Usalama katika Wilaya zao ni shwari na wananchi wanaendelea na shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kiuchumi.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.