• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

RC KUNENGE AWAAPISHA WAJUMBE WA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA SASA RASMI HUDUMA KUPATIKANA KIBITI.

Posted on: March 28th, 2024

Baada ya kukosekana kwa Baraza la ardhi na nyumba kwa muda mrefu Wilaya ya Kibiti hatimaye jana tarehe 27.03. 2024 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge akiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo amewaapisha wajumbe wawili wa Baraza hilo ambao wanakwenda kuanza majukumu yao kuanzia sasa. Walioapishwa  ni Ndg. Salum Mkeyenge  na Bi. Mariam Sinahofu wote wakiwa ni wakazi wa Kibiti.

Mara baada ya kufanyika uapisho huo mbali na pongezi kwa wajumbe hao Mhe. Kunenge amewataka wakafanye kazi kwa nguvu zao zote kadri ya uwezo wao kwa kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi kwani hakuna aliye juu ya sheria.

"Uteuzi huu umefanyika kwa mujibu wa Sheria, mmeaminiwa na kuteuliwa kuwahudumia wananchi, kafanyeni kazi" Alisema Kunenge.

Vilevile Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwa kupatikana kwa  Baraza la ardhi na nyumba Wilaya ya Kibiti ni matarajio yake migogoro ya ardhi itapungua ama kutokomezwa kabisa huku akisisitiza Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha hakuibuliwi  migogoro mipya.


"Mkurugenzi simamia isizalishwe migogoro mipya, ni matarajio yangu tunakwenda kupunguza na kumaliza changamoto hii" Alisema Kunenge.

Hata hivyo Mhe. Kunenge amesema kupatikana kwa Baraza hilo Wilaya ya Kibiti, sasa linakwenda kufanya Wilaya zote za Mkoa wa Pwani kuwa na mabaraza hayo ikiwa ni sehemu ya kutekeleza  mpango wa Serikali kuhakikisha kila Wilaya inakuwa na mabaraza ya ardhi na nyumba.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema kuanzishwa kwa Baraza la ardhi na nyumba katika Wilaya yake ni faraja kubwa kwani sasa kesi zote zitatatuliwa ndani ya Wilaya na walengwa kupata haki zao bila kutumia gharama kubwa ambapo awali walilazimika kusafiri kwenda Wilaya jirani ya  Mkuranga kupata huduma hiyo.


"Nimefarijika sana Baraza hili kuanzishwa Kibiti, sasa wananchi wangu watapumzika na safari na gharama walizokuwa wanatumia kwenda kutafuta haki zao Mkuranga". Alisema Kanali Kolombo.

Aidha Msajili msaidizi wa mabaraza ya ardhi na nyumba Mhe. Mwendwa Mgulambwa ameeleza kuwa moja ya kazi kubwa ambazo wajumbe hao watafanya ni kutoa huduma ya kusikiliza, kushauri na kutatua migogoro yote ya ardhi Wilayani Kibiti.

Naye Mkuu wa kitengo cha Sheria wa  Mkoa Mhe. Marcelin Ndimbwa amesema, kutokana na migogoro ya ardhi iliyopo, kuapishwa kwa wajumbe hao ni muhimu katika jamii na wanakwenda kumsaidia Mkuu wa Mkoa majukumu aliyopewa na Mhe. Rais. wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. SSH.

Wateule walioapishwa leo Ndg. Salum Mkeyenge na Bi. Mariam Sinahofu wamesema wameshukuru kwa kuaminiwa na kuteuliwa hatimaye Leo kuapishwa hivyo watasimamia vyema na kuhakikisha haki inatendeka. Pia wamesisitiza kuwa wapo tayari  kusikiliza wananchi kwa weledi mkubwa ili kuweza kutambua chanzo cha matatizo na kwa nafasi zao waweze kushauri na kutoa maamuzi kwa haki zinazostahiki.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.