• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SHEREHE ZA KILELE CHA SIKU YA WANAWAKE KIBITI ZAHITIMISHWA KATIKA UWANJA WA SAMORA.

Posted on: March 8th, 2024

8.3.2024.

Wanawake wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti wameungana na Wanawake wengine duniani kote kusheherekea siku ya wanawake Duniani ambayo huadhimisha kila mwaka ifikapo Machi 8.

Maadhimisho hayo ni mahususi kwa kutoa hamasa kwa Wanawake kuweza kijitathmini kimaendeleo katika ngazi ya uchumi, Siasa na kiutamaduni ili kuleta chachu ya usawa wa kijinsia pia kujitafakari mahali walipotoka , walipo sasa na wanapoelekea.

Akisoma risala mbele ya Mgeni rasmi Afisa Maendeleo ya jamii Irene Urasa amesema kupitia kauli mbiu ya mwaka huu isemayo " Wekeza kwa mwanamke, kuharakisha maendeleo ya Taifa na ustawi wa jamii" imelenga kuhamasisha jamii kuwekeza kwa mwanamke zaidi kwani mwanamke ni Mlezi na mzalishaji katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na akikwamuliwa mmoja ni sawa na kuwezesha Taifa zima.

Pamoja na jitihada zinazofanywa na Serikali Bado kuna changamoto mbalimbali Wilayani Kibiti zinazoendelea kuwakabili wanawake ikiwa ni pamoja na mfumo dume, kutothamini mchango wa mwanamke kwa baadhi ya wanajamii  na kushindwa kujikwamua kutokana na ukosefu wa mitaji.

Hata hivyo Bi Urasa amesema kutokana na changamoto hizo wanapendekeza jamii kuelimishwa kutambua mchango wa wanawake, faida za kuwekeza na hasara ya kutowekeza kwa wanawake. 


Historia inaonyesha maadhimisho hayo yalitokana na jitihada za wanawake 15,000 ambao waliandamana mjini New York huko nchini Marekani wakidai kupunguziwa muda wa kazi, kupatiwa ujira wa kuridhisha na kupata haki ya kupiga kura.


Kabla ya Mgeni rasmi kuongea na halaiki ya wanawake waliojitokeza kwenye maadhimisho hayo, Diwani wa Maparoni mhe. Bakari Mpate  kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri amesema Baraza la Wahe. Madiwani Wilaya ya Kibiti linapambana na litaendelea kupambana kuhakikisha 10% ya mapato ya ndani inawafikia wanawake, vijana na walemavu kwa kutoa mikopo kama ilivyoelekezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Akimwakilisha Mgeni rasmi Kaimu Katibu Tawala Ndg. Salim Malogwa amesema jamii inapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali kuweza kusaidia upatikanaji wa haki za Msingi za Wanawake bila kujali hali zao ili kuweze kuleta maendeleo chanya katika uchumi na Ustawi wa Jamii. 

Hata hivyo amesisitiza kuwa katika kuhakikisha kuwa haki hizo zinapatikana ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha wanawake wanawezeshwa zaidi na kuwa sehemu ya ushindani katika uchumi wa Teknolojia ili waweze kushiriki katika shughuli za maendeleo  katika nyanja mbalimbali.

Mwisho Bw. Malogwa amesisitiza wanawake kutumia Teknolojia kwa mtazamo chanya ili waweze kupiga hatua zaidi katika masuala mbalimbali hususani katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.