• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SHULE YA MSINGI MNG’ARU YAPATA NEEMA YA CHAKULA KWA MWAKA MZIMA.

Posted on: February 14th, 2023

Tarehe 14/02/2023 Taasisi ya Youth Crossing Boundaries Foundation (YCB) yenye ofisi zake Wilaya ya Ubungo kata ya Manzese Jijini Dar es salaam, Ikiongozwa na Mkurugenzi wake Bw. Alphonce Leonard imetembelea shule ya msingi Mng’aru  iliyopo kata ya Dimani  Wilaya ya Kibiti kwa lengo la kuonyesha upendo kwa Wanafunzi 120 wa shule hiyo kwa kuwachangia unga, Rimu papers, vikombe, pamoja na sukari.

Taasisi hiyo  inayojihusisha pia na kuwasaidia wanafunzi Mashuleni na hasa masuala yanayohusu afya zao, inatarajia kuingia mkataba na Uongozi wa Shule hiyo ili kuweza kufadhili unga na sukari kwa ajili ya uji wa wanafunzi wa shule hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kama ambavyo walifanya mwaka uliopita katika shule ya msingi Kinyamale iliyopo kata ya Bungu Wilayani Kibiti.

“Leo ikiwa ni siku ya wapendanao tumechagua kuja hapa kuonyesha upendo kwa Watoto hawa, na tumekuja na zawadi kidogo kwa ajili yao ili kuunga jitihada za Mhe. Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kuchangia unga ,sukari na vikombe.” Alisema hayo Bw. Alphonce.

Aliendelea kusema “Ikiwa shule itaridhia tutaingia Mkataba wa kuchangia unga na sukari kwa ajili ya uji hivyo tutahitaji kupata bajeti ya mwezi ili kujua gharama za kuhudumia kwa mwaka mzima.”

Hatahivyo Mkurugenzi wa Taasisi hiyo alitoa wito kwa wazazi na walezi wa wanafunzi kuendelea kuchangia huduma za chakula cha mchana shuleni ili kuwajengea wanafunzi uwezo mzuri wa kustahimili masomo yao na kuongeza ufaulu.

Naye Diwani wa kata Hiyo Mhe. Yusuph Mbinda, alieleza kuwa wanafanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha agizo linatekelezwa na chakula kinapatikana shuleni siku zote wanafunzi wawapo shuleni.

“ Sisi kama Kijiji hatujakaa kimya juu ya suala hili hivyo katika kuunga juhudi za Mhe. Rais, tumesafisha shamba lenye ukubwa wa ekari 3 kwa ajili ya kupanda ufuta wa shule utakao saidia ununuzi wa Chakula baada ya mavuno. Hivyo tunategemea suala la njaa kwa wanafunzi wetu shuleni litakuwa historia ” alisema Diwani.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO:SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

    June 12, 2025
  • PPRA KANDA YA PWANI YATOA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA NA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA

    June 12, 2025
  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.