• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: December 25th, 2022

Idara ya Maendeleo ya jamii jinsia Wazee na watoto Wilaya ya Kibiti kwa kushirikiana na wadau mbalimbali washeria,wamefanya uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsi kwa wanawake na watoto duniani Katika Kata ya Bungu B, ambayo huadhimishwa Kila mwaka kuanzia novemba 25 mpaka Disemba 10 ulimwenguni.

Maadhimisho hayo ambayo mwaka huu kauli mbiu ya Kitaifa ni KILA UHAI UNA THAMANI, TOKOMEZA MAUAJI NA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO huazimishwa kwa lengo la kufanya kumbukuzi ya kuwaenzi akina dada wa Mirabal, wanaharakati watatu wa kisiasa kutoka Jamhuri ya Dominika ambao waliuawa kikatili mwaka 1960.

Lengo la Umoja wa Mataifa kupitisha kuadhimishwa kwa siku ya ukatili Duniani ni  Kuongeza uelewa wa umma juu ya suala hilo kila mwaka ifikano 25 Novemba na kuhitimishwa Disemba 10 ambapo ulimwengu huadhimisha siku ya haki za binadamu ikiwa ni nafasi nzuri ya kuweza kupaza sauti na kusikika ulimwengu mzima.

Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Mhe. Ramadhani Mpendu, Mwenyekiti wa kitongoji cha Kibaoni  Bungu B Ismaii Mikoi amesema ni wajibu wa Kila mtoto kutoa taarifa anapofanyiwa ukatili wa aina yeyote ile.

Hata hivyo Mikoi amewasihi watoto kuacha tabia ya uoga akisisitiza kutoa taarifa ni muhumu kuanzia nyumbani mpaka ngazi ya juu ili wahusika wachukuliwe hatua stahiki za kisheria .

“ watoto ni viongozi wa baadae fungukeni kutoa taarifa mnapona viashiria au mnapifanyiwa ukatili,  tunahitaji kuwa na kizazi chenye Afya Bora”alisema Mikoi.


Aidha amewataka watoto kuwa na tabia ya kutembea kwa makundi hususani katika muda wa kwenda shule, huku akisisitiza kuepuka kutembea mmoja mmoja kwani kumekuwa na matukio ya watoto kupotea, kufanyiwa vitendo viovu na kuuawa kikatili.

Vilevile amewaambia watoto wanapoona mtu anawafatilia na hawamfaahamu wakimbie kutoa taarifa wasikubali kufuatana nao au kuwasikiliza watu wa aina hiyo, lolote na wakiona hawezi kukimbia wapige kelele watu wawasaidie.

Pia amesema hata kama ni mtu mnamfahamu anakuwa na dalili hizo usiogope, toa taarifa au mpigie kelele anapojaribu  kukufanyia ukatili.

Aidha amesema kutokana na elimu iliyotolewa kuhusu ukatili wa kijinsia  ni imani yake watoto wameelewa na anatarajia kupokea taarifa kwa kila atakayefanyiwa ukatili wa kijinsia muda wowote ule .

Uzinduzi wa ukatili wa kijinsia uliambatana na burdani kwa  michezo mbalimbali kama vile maigizo,kwaya ,mpira wa miguu,kukimbia kwa gunia na kukimbiza jogoo.


 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO:SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

    June 12, 2025
  • PPRA KANDA YA PWANI YATOA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA NA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA

    June 12, 2025
  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.