• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SIKU YA MTOTO WA AFRIKA YAFANA, TAASISI ZA KEF NA CAMFED ZATOA ZAWADI KWA WATOTO KIBITI.

Posted on: June 18th, 2024

Siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 16.6 ikiwa ni kumbukizi muhimu kwa ajili ya watoto wa Kitongoji cha Soweto nchini Afika Kusini waliouawa kutokana na ubaguzi wa rangi. Watoto hao walikuwa wakidai haki zao za kibinadamu ikiwemo kutobaguliwa na haki ya kupata elimu bora hivyo kupinga mifumo ya elimu ya kibaguzi. Kutokana na tukio hilo uliokuwa umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) uliazimia kuwa tarehe hii kila mwaka iwe Siku ya Mtoto wa Afrika.


Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti imeungana na nchi nyingine za Afrika kuadhimisha siku hiyo katika viwanja vya shule ya Msingi jaribu mpakani, sherehe ambayo ilipambwa kwa burudani mbalimbali kutoka kwa watoto kama vile kwaya, igizo, shairi, ngoma n.k zenye jumbe muhimu kuhusu watoto ikiwa ni pamoja na kupewa haki zao za msingi.

Siku ya mtoto wa Afrika Mwaka 2024 imebeba kaulimbiu yenye ujumbe maalum usemao "ELIMU JUMUISHI KWA WATOTO IZINGATIE MAARIFA,MAADILI NA STADI ZA KAZI".

Katika maadhimisho hayo Mgeni rasmi Katibu Tarafa wa Kibiti Ndg. Salum Mzaganya kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo amesema, Mkuu huyo amewaagiza wazazi kuhakikisha wanawalea watoto wao katika maadili, kuwalinda na kuwapatia mahitaji yao ya Msingi. Pia ameiagiza Taasisi zinazohusiana na ulinzi wa watoto kuchukua hatua kali kudhibiti matukio sambamba na jamii kutoa taarifa za ukiukwaji wa haki za watoto kama vile ubakaji, ulawiti n.k. pia Mkurugenzi Mtendaji kuwa na bajeti kwa ajili ya shughuli za ulinzi wa mtoto.

Awali akimkaribisha Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg. Hemed Magaro alisema, kutokomeza ukatili kwa watoto si suala la mtu binafsi bali ni jukumu la jamii nzima kwa ujumla kusimamia malezi ya watoto hao.

Aidha katika risala ya watoto hao waliohudhuria ilieleza kuwa watoto wamependekeza wazazi na walezi kuelekezwa namna ya kutimiza wajibu wao, kuchukua hatua kali kwa wanaowafanyia ukatili, elimu ya ukatili na lishe kuwa endelevu ikiwa ni pamoja na Serikali kuweka Mazingira rafiki katika shule na kusimamia upatikanaji wa chakula mashuleni.

Mwisho katika sherehe hiyo Taasisi ya Kalamu Education Foundation na CAMFED walitoa zawadi za vifaa  mbalimbali kwa watoto walichaguliwa kujiunga na kidato cha tano, taulo za kike kwa mabinti pamoja na sabuni ya unga ya kufulia.

Wageni mbalimbali walihudhuria sherehe hiyo wakiwemo wale kutoka Taasisi ya kidini ya KKKT Dayosisi ya Pwani na Mashariki, pamoja  Paralegal kutoka  Ilala na Kinondoni.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.