• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

Siku ya pili ya Mkutano wa WETLANDS na wadau

Posted on: November 18th, 2022


SIKU YA PILI

Hatimaye muafaka wa jinsi gani Shirika la Wetland international litashirikikiana na jamii kulinda na kuhifadhi misitu ya mikoko delta ya rufiji katika Wilaya ya kibiti umepatika kwa kupitisha  maadhimio mbalimbali yatakayoanza kutekelezwa rasmi mwakani baada ya wadau kutoa maoni na kukubaliana.

Hayo yamebainishwa katika majadiliano yaliyodunu kwa siku 2 katika ukumbi mikutano wa Halmashauri Wilaya ya Kibiti ambapo wadau wamekubaliana utekekezaji wa kuhifadhi mikoko kuanza sasa sambambakuzitaka mamlaka husika kupitia upya sheria za uhifadhi wa mikoko na  delta na kuunda sheria ndogo, kwa kuweka  kipaumbele cha uhifadhi shirikishi kwa kipindi cha miaka 30 huku wakisisitiza viongozi wote wa delta kusimamia majukumu yao ipasavyo. Pia wameitaka  Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kutoa  wataalamu wao kutekeleza majukumu yaliyoainishwa ambayo wakisaidiana  na Taasisi ya wetland ili jamii itambue faida zitokanazo na mikoko.

Ili kufika malengo ndani na nje ya delta Kwa miaka 30 ijayo,wanarsha wamekubaliana kutoa Elimu Kwa jamii kujua faida ya mikoko Kwa njia ya maigizo,vipeperushi na mikutano ya hadhara,kubaini na kuweka mikakati ya kulinda na kuhifadhi maeneo ambayo hayajaathirika,kubaini na kurejesha uoto wa asili kwa maeneo yaliyoathirika,kuanzisha njia mbadala za kiuchumi kama vile kilimo,ufugaji wa nyuki,utalii na uvuvi wa kisasa ikiwa ni pamoja na kuanzisha mfuko maalum kwa lengo la kulinda na kuendeleza uhifadhi wa mikoko na kuziwezesha jamii zinazoishi delta.

Vilevile katika mjadala huo wadau wamesema kinachochangia kuharibu uoto wa asili kwa maeneo ya delta ni pamoja na kufanyika kwa shughuli za uvunaji wa mbao kwa kukata mikoko,uvamizi wa idadi kubwa ya wafugaji,kilimo cha mpunga kisicho rafiki,utupaji taka na uchomaji wa moto ndani ya misitu.Wakati huo huo wakakubaliana kufanyika marekebisho Kwenye Sheria kubwa na ndogo za kudhibiti aina zote za uvuvi haramu kwa kufanya doria,pia kufanyika marekebisho kwenye Miradi inayotekekezwa na itakayotekelezwa  pamoja na kuiwezesha kamati ya maliasili na TFS kushirikiana katika utekekezaji.

Hata hivyo wanawarsha wamesema Ili kuhifadhi mikoko Kuna Kila sababu ya uhitaji wa kuimarisha usimamizi wa mikoko,kuimarisha huduma za kijamii maeneo ya delta,kutoa elimu ya uvuvi endelevu, ufugaji endelevu na kilimo endelevu  chenye tija,pia kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo na kutunga sera itakayowezesha kufanya biashara ya hewa ukaa.

Aidha eneo la Pwani ya Rufiji linatarajiwa kunufaika na  asilimia 30 ya mapato yatokanoyo na shughuli za uhifadhi wa mikoko Kwa ujumla hivyo wadau hao wameiomba Serikali kuzuia na kuondoa mifugo maeneo ya delta, kusimamia uendeshaji wa misitu na uhifadhi wa mikoko,kuboresha miundombinu ya barabara ,mitaro na umeme ikiwa ni pamoja na kutambua thamani ya na (mtu binafsi) vinavyohusika na uhifadhi wa mikoko.

Wetland international ni shirika/taasisi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na kazi ya kulinda na kuhifadhi ukanda wa  ya delta ya Rufiji Tanzania katika maeneo oevu hususani katika Wilaya ya kibiti ambapo kati ya aina 7 ya mikoko inayopatikana bara la Afrika 6 hupatikana kibiti pekee.ukiacha Tanzania Wetland international hufanya kazi na nchi za Uganda,Sudan kusini, Ethiopia na Senegal.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.