• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAFANA WILAYANI KIBITI.

Posted on: March 7th, 2023

Tarehe 7.3.2023 

Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti imeungana na nchi nyingine  ulimwenguni kusheherekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani katika uwanja Samora Wilayani humo  na kuhudhuriwa  na viongozi wa serikali, Chama, Taasisi na wananchi mbalimbali bila kuwasahau Wanafunzi.

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, yalianza  kuadhimishwa kuanzia tarehe 02/03/2023 na kufikia kilele tarehe 08/03/2023 kwa kunogeshwa na  Kauli mbiu ya mwaka huu ni isemayo “UBUNIFU WA MABADILIKO YA TEKNOLOGIA NI CHACHU KATIKA KULETA USAWA WA KIJINSIA”.

Historia ya maadhimisho haya ni matokeo ya vuguvugu la wafanyakazi wanawake elfu kumi na tano walioandamana mwaka 1908 jijini New York Marekani wakidai kupewa muda mfupi wa kufanya kazi, malipo bora na haki ya kupiga kura ambapo wazo la siku hii lilitolewa mwaka 1910 na mwanaharakati wa kikomunist mtetezi wa haki za wanawake Bi Clara Zetkin.

Katika maadhimisho hayo yaliyoanza kwa maandamano na kupokelewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti mhe. Ramadhan Mpendu mbaye alikuwa ndiye mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amesema, kuwawezesha wanawake kuingia katika Viwanda vidogo vidogo kunaongeza ubunifu kwenye Shughuli wanazofanya kulingana na mabadiliko ya teknologia.

Vilevile Mhe. Mpendu amesema, wanawake wana mchango mkubwa katika maendeleo ya familia na Taifa Kwa ujumla, hivyo bado tunajukumu kubwa kama Serikali la kuelimisha jamii kutambua, kuheshimu na kuthamini suala la USAWA.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo amesisitiza kuwa, kuwawezesha wanawake kuwa na mazingira mazuri ya kisheria kutasaidia kutatua changamoto zinazojitokeza katika kaya mbalimbali nchini, huku akizikumbusha jamii kutambua na kujua umuhimu wa kuwawezesha wanawake, kushiriki katika michakato ya Shughuli za maendeleo ili kuleta maendeleo chanya Kwa wananchi kiuchumi na kijamii kwa ujumla.

“Wanawake ni watu muhimu sana katika jamii, wapewe kipaumbele katika kuwawezesha kielimu, kiuchumi, kisiasa na kijamii” Alisema Mpendu.

Aidha ili kuleta MABADILIKO ya maendeleo kibiti Mpendu ambaye pia ni Diwani wa Bungu, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, jambo litakalo wasaidia kupanuka kimawazo na kupata haki zao za Msingi.

Katika sherehe hiyo Katibu wa chama cha Walimu Mwl. Crecencia Tindwa amewataka wazazi kuwa na tabia ya  kufuatilia mwenendo wa watoto katika masomo yao ikiwa ni pamoja na kukagua madaftari yao, huku akiwasisitiza wanawake kupendana, kujiendeleza kielimu na kujifunza vitu vipya na vizuri kutoka kwa wengine.

Vilevile Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Wilaya ya Kibiti Latifa Augustino amewasihi wanawake kufanya kazi Kwa bidii, kujituma na kuwa na tabia ya kuweka akiba sambamba na kuwekeza kwa manufaa ya baadaye. Pia afisa ustawi wa jamii Ansila akatoa elimu ya malezi Bora ya watoto wao na kuwapa huduma muhimu wakati Patricia Mdemu kutoka NGO’s ya Jicho angavu na msaada wa kisheria akitoa elimu juu ya ndoa na haki zake za msingi.

Naye mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibiti bi Tatu mkumba katika maadhimisho hayo ameitaka Jamii kupinga ukatili wa kikinsia kwa nguvu zote Wakati Diwani wa Kata ya Kibiti Mhe. Hamidu Ungando Yeye amesema kuna kila sababu ya kusimamia ustawi wa kina mama waweze kujikwamua kwani kina mama ni viongozi.

Awali mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi Raya Mlawa mwandishi wa vikao (CC) wa Halmashauri ya kibiti alisema   shughuli zilizofanyika katika kuadhimisha ni pamoja na kufanya usafi katika kituo cha Afya kibiti , kuwafariji wagonjwa katika wodi ya wanawake, watoto na wanaume na kutoa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi wa kike waliofanya vizuri shule ya sekondari Mjawa.

Pia sherehe hiyo ilitumbuizwa kwa kufanya maonesho ya shughuli za vikundi vya ujasiriamali, kupima uzito na kupewa ushauri na kufanya igizo la rushwa ya ngono makazini lililoshirikisha ushiriki wa Taasisi ya kupambana na Rushwa TAKUKURU.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.