• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

TAMASHA LA AFYA LAFANA KIBITI – WANAUME, WANAWAKE NA VIJANA WAJITOKEZA KUCHANJA

Posted on: February 11th, 2024

7.2.2023

Idara ya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kwa kushirikiana na shirika la Chuo Kikuu cha Johns Hopkings kupitia mradi wa Breakthrough Action wamefanya Tamasha kubwa la kuhamasisha jamii kwa kutoa elimu ya umuhimu wa chanjo mbalimbali katika viunga vya stendi ya mabasi Kibiti tarehe 7 Februari, 2024.

Licha ya kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa chanjo na uchanjaji wa chanjo za aina mbalimbali pia wameendesha zoezi la vipimo vya magonjwa mbalimbali kama vile malaria Upungufu wa Kinga Mwilini/ UKIMWI pamoja na kuchangia damu.

Katika Tamasha hilo Taasisi hiyo imetumia jukwaa la  Mashindano ya nusu fainali ya kombe la Afrika (AFCON) kuelimisha Jamii hususani kwa  kuwalenga  wanaume  kuweza kujua zaidi umuhimu wa chanjo.

Kauli mbiu ya Tamasha hilo  imevinjari na kibwagizo kisemacho " kuwa bingwa ambaye familia yako inahitaji" Chanjo ni Afya, Onesha Upendo pata chanjo na mpeleke mtoto akachanjwe .

Wakitoa utambulisho wa ugeni huo, Katibu Tawala wa Wilaya , Mkurugenzi Mtendaji na Mganga Mkuu, kwa nyakati tofauti wameipongeza Taasisi hiyo kwa kuona umuhimu wa kutoa elimu ya chanjo huku wakiwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi na kutumia fursa hiyo kupima ,kuchanja na kuchangia damu.

"Leo tumepata ugeni mkubwa, ndg Wananchi jitokezeni kwa wingi kutumia fursa hii njooni mpate chanjo na mpime Afya zenu" Walisema Viongozi hao.

Akimuwakilisha Mgeni rasmi Dr.Festo Ndugange Naibu Waziri Tamisemi, Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema Serikali imekuwa na juhudi kubwa, kuhakikisha inadhibiti magonjwa ya milipuko na yasiyo ya milipuko kwa kutoa chanjo kama vile, Pepopunda, Ndui, Polio, Uviko19 (Korona) n.k.

Kanali Kolombo aliendelea kusema kwamba katika awamu zote za Uongozi wa viongozi Tanzania, Serikali imeendelea kushirikiana na wadau wa Afya kutoa huduma kwa kutumia Afua zote  kudhibiti na kupunguza vifo kwa wananchi hususani miaka ya 2020 katika mlipuko wa ugonjwa wa “COVID 19” na kazi inaendelea.

Kufuatia hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali Kanali Kolombo amewasisitiza Wananchi wa Kibiti kuendelea na utaratibu wa  kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya magonjwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na  Kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni, Kula chakula cha moto ili kuweza kujinga na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu,  Kufanya mazoezi sambamba na kula Lishe Bora kwenye familia.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya na Mgeni rasmi katika Tamasha hilo, amewataka  watalaam kuendelea kufanya tafiti nyingi ili kupata chanjo na dawa madhubuti dhidi magonjwa  yanayosumbua wananchi kwa  wingi kama Malaria, Mfumo wa kupumua, Upungufu wa damu na mengineyo.

Mwisho Kanali Kolombo  amempongeza Mhe Rais Dkt. SSH kwa kuona umuhimu wa chanjo nchini huku akiipongeza wizara ya Afya kwa ushirikiano mzuri na wadau jambo ambalo litaendelea kuimarisha huduma na kufikia malengo ya kuwa Taifa lenye Afya Bora.

Nao viongozi wa Chama waliohudhuria Tamasha hilo wamemshukuru Rais Dkt. SSH kwa kufanya kazi kwa karibu na jamii na kuwasogezea huduma ambapo pia wamepata elimu. Kupitia mashindano hayo ya AFCON Tamasha limewasogeza wanaume wengi kushiriki kwakuwa wanaume hupenda mchezo wa soka.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.