• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

TTCL YABISHA HODI KIBITI, MKONGO WA TAIFA KUANZA KAZI MWEZI MEI MWAKA HUU.

Posted on: March 14th, 2024

Wakati jengo la Ofisi ya kituo cha mkongo wa Taifa wa mawasiliano Wilaya ya Kibiti likiwa imekamilika kwa  95% Viongozi wa Kampuni ya simu Tanzania TTCL wamewasili wilayani humo kwa lengo la kutoa uelewa juu ya matumizi ya mkongo huo unaotarajiwa kuanza kutumika mwezi mei mwaka huu baada ya ujenzi huo kukamilika.

Akizungumza na Kamati ya ulinzi na Usalama pamoja na  Wakuu wa Idara na vitengo Afisa Mkuu Ofisi ya mkongo wa Taifa makao makuu Bw. Edson Richard amesema, wamefika Kibiti kwa lengo la kutoa uelewa kwa sababu wameongeza njia za mkongo ambapo awali  Wilaya ya Kibiti haikupitiwa na mkongo huo.

Vilevile ndg Richard amesema, Serikali imejenga mkongo wa Taifa kwa madhumuni makubwa ya kujenga uchumi na jamii habari (information society) ambao kazi yake kubwa ni kusafirisha mawasiliano yote nchini kama vile, maongezi ya simu, huduma ya internet, taarifa mbalimbali za ujumbe mfupi (sms), huduma za kifedha kama vile kutuma na kupokea pesa kwenye simu (mobile transfer money), radio na television sambamba na kuwezesha ufanisi wa huduma za mawasiliano kwenye Taasisi za fedha (bank na ATM).

Naye Meneja wa huduma kwa wateja TTCL  Bi. Wendlyne Mbagga amesema, kupitia makampuni yaliyosajiliwa kutoa huduma za simu na  internet miundombinu ya mkongo wa Taifa wa mawasiliano utatumika kutoa huduma za kisasa za utumaji na upokeaji wa taarifa pamoja na kurahisisha utoaji wa huduma za Afya mtandao (e - health), elimu mtandao ( e - learning), kilimo mtandao ( e - agriculture) Serikali mtandao( e - government) n. K.

Aidha Bi. Wendlyne amesema kupitia huduma hizo wananchi katika maeneo mbalimbali watafaidika kwa sababu huduma za mawasiliano zitaimarika,  ajira zitaongezeka na vipato vitaongezeka kwani kutafanyika biashara kama vile m pesa, tigo pesa, mawakala wa mabenki mbalimbali n.k


Mara baada ya kupokea ugeni huo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo ameishukuru  kampuni ya simu ya TTCL kwa ujio wake mzuri, huku akikiri maendeleo ya mawasiliano yanaonekana ukilinganisha na ilivyokuwa awali pamoja na kumpongeza Mhe. Rais Dkt SSH kwa juhudi anazozifanya kuhakikisha kila Mtanzania anapata mawasiliano popote alipo.

Mbali na hayo Kanali Kolombo amesema ujio wa mkongo wa Taifa Wilaya ya Kibiti ni faraja kubwa kwa wakazi wa Kibiti kwani pamoja na uwepo wa mawasiliano kuna baadhi ya maeneo bado yana changamoto, na ni Imani yake kwamba Sasa  kero hiyo inakwenda kupata mwarobaini.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.