• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

VYAMA 6 KATI YA 7 VYATEULIWA KUPEPERUSHA BENDERA ZAO UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI KATA YA MAHEGE.

Posted on: July 1st, 2023


Msimamizi  wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo Bw. Hemed S. Magaro  tarehe 30 June, 2023 amewateua watu sita kuwa wagombea wa udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa Kata ya Mahege iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.

Wagombea hao na vyama vyao kwenye mabano ni pamoja na Bw. Seif Adam Mkokwa (UMD), Bw. Musa Juma Maramuah (UDP), Bw. Sultani Said Mpondi (UPDP), Bw. Mrisho Miraji Jongo (CUF), Bw. Hamada Juma Hingi (CCM) na Bw. Sadick Athumani Mzuzuri (NRA)

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kampeni kwa ajili ya Uchaguzi Mdogo kwenye kata hiyo zitaanza  tarehe 01 hadi 12 Julai, 2023 na uchaguzi utafanyika tarehe 13 Julai, 2023.

Tuligawa fomu kwa vyama  7 kwa mujibu wa sheria  mpaka June 30,  saa 10 :00 jioni, vyama 6 vimerejesha fomu na vyote kuteuliwa kusimamisha wagombea , hivyo kuanzia tarehe 1 - 12 Julai kampeni zinaanza,  wananchi jitokezeni  kuchagua viongozi wenu kwa amani na utulivu "Alisema Magaro.

Katika zoezi hilo Msimamizi wa uchaguzi Bw. Hemed Magaro amewaagiza wenyeviti wa vijiji kuitisha mkutano wa halmashauri ya vijiji vyao Ili kuweza kuhamasisha na kuwajulisha wananchi juu ya zoezi la uchaguzi litakalofanyika julai 13 mwaka huu.

Vilevile Magaro amewaagiza watendaji wa Kata, wenyeviti wa vijiji na vitongoji kutoa taarifa  mapema wanapohisi au wanapopata taarifa za viashiria vya uvunjifu wa amani.

"Zoezi hili ni la kitaifa, macho yote ya nchi yako hapa, watendaji ngazi ya Kata, vijiji na vitongoji mna wajibu mkubwa kuhakikisha mnasimamia vizuri uchaguzi huu kwa kufuata Sheria ,kanuni ,na taratibu za uchaguzi kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru, wa haki na amani ili democrasia izidi kuimarishwa" Alisema Magaro.

Aidha Mkurugenzi Msaidizi wa Habari kutoka Tume ya uchaguzi Bi. Leila Muhaji, amewataka Viongozi wa vijiji katika siku zilizosalia kuhakikisha wanatoa matangazo  kupitia njia mbalimbali zitakazoweza kuwafikia na kuwajulisha wananchi kujitokeza kupiga kura kulingana na uzoefu wa mazingira yao.

"Tupo hapa kuhakikisha zoezi la uchaguzi linakamilika kama ilivyokusudiwa, watendaji Kata, wenyeviti wa vijiji na vitongoji tunaomba ushirikiano wenu " Alisema Leila Muhaji.

Hata hivyo  Viongozi hao waliainisha njia za matangazo ziltakazotumika  kuwafikia wananchi wote kuhusu taarifa ya uchaguzi ikiwa ni  pamoja na  njia ya Kigoma (lamgambo), redio, gari la matangazo, na kuitisha kikao cha kamati ya Kijiji katika vijiji vyao kuwaeleza wananchi kuhusu uchaguzi huo.

Mara baada ya majina kubandikwa kwa nyakati tofauti wagombea wa vyama vyote wamewapongeza Tume ya Uchaguzi ,Viongozi wa Wilaya kwa namna walivyowapokea vizuri , kwa jinsi walivyo waelimisha na mwisho zoezi hilo kwenda vizuri bila kasoro yeyote mpaka sasa. Pia wagombea hao wameomba wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha uchaguzi unasimamiwa kwa haki. Hata hivyo wagombea walisema kuwa  wapo tayari kutoa ushirikiano na kumuunga mkono atakayechaguliwa kuiongoza Kata ya Mahege.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.