• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WADAU WA ELIMU KIBITI WATOA AHADI YA MADAWATI 40, MEZA 50, VITI 70 NA TSH. 750,000/= ILI WANAFUNZI WASIKAE CHINI.

Posted on: January 18th, 2024

Jana 17 Jan 2024, Mkuu wa wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo ameongoza kikao cha wadau wa Elimu wilayani Kibiti ili kuweka mikakati na kushirikishana mambo mbalimbali yanayoihusu sekta ya Elimu wilayani humo kwa mwaka 2024. 

Katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji, Afisa Elimu Msingi na Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya ya Kibiti kwa nyakati tofauti walieleza mafanikio waliyopata kwa mwaka uliopita 2023, Mipango na mikakati iliyopo kwa mwaka huu 2024 upande wa Halmashauri pamoja na changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

Changamoto kubwa iliyoonekana hasa kipindi hiki cha kufungua shule ambapo wanafunzi wapya wanasajiliwa mashuleni ni upungufu wa madawati upande wa Elimu Msingi na viti na meza kwa upande wa Elimu Sekondari.


Kuhakikisha changamoto hii inaisha wadau hao walitoa ahadi ya michango ya Madawati 40, Meza 50, Viti 70 na fedha Tsh. 750,000 huku wengine wakiahidi kuleta kadri watakavyopata na kuweka azimio la kuendelea kuomba kutoka kwa wadau wengine wasiohudhuria na wale wenye mapenzi mema na mustakabali wa Elimu wilayani Kibiti.

Aidha moja ya mkakati uliowekwa na wadau hao ni kuhakikisha Halmashauri inajenga miundombinu kwaajili ya shule ya sekondari itakayochukua Kidato cha Tano na Sita.

“Upande wa Elimu ya Awali na Msingi tayari tumefanikiwa tuna shule za kutosha, lakini upande wa sekondari hatuna shule hata moja ya ‘Advance’ sijui tunafeli wapi” Alihoji Mjumbe mmoja


Akijibu hoja hiyo Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Hemed Magaro alisema Halmashauri tayari ina mpango na wanatenga bajeti kwaajili ya kufanikisha hilo,  moja ya shule ambazo ziko kwenye mpango huo ni shule ya sekondari Dimani.


“Moja ya sifa ya shule za ‘Advance’ ni mabweni, shule zetu nyingi tayari zina madarasa ya kutosha pamoja na maabara lakini hatuna mabweni, tukifanikiwa kupata mabweni na miundombinu mingine saidizi hata sasa tunaweza kuiombea usajili ikawa ‘Advance School’” Alisema Magaro

Kanali kolombo alihitimisha kwa kuwashukuru wadau kwa michango na ahadi zao huku akitoa rai kwa watu wote tuendelee kuichangia Halmashauri yetu hata kama ni Kilo moja ya misumari, tuhakikishe Sekta ya Elimu inafanya vizuri Kibiti na watoto wetu wanapata Elimu stahiki.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.