• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WADAU WA ELIMU KUTAFUTA MWAROBAINI WA KUSHUKA KWA UFAULU WILAYANI KIBITI

Posted on: January 25th, 2023

Wadau wa maendeleo ya elimu wa Wilaya ya Kibiti wamekutana katika ukumbi wa shule ya sekondari kibiti kujadili na kupata mwarobaini wa mapinduzi ya elimu kwa kujitathmini, kujipanga  Pamoja na kupata mbinu mbalimbali za  kuweza kuinua hali ya ufaulu ndani ya Wilaya .

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya elimu Afisa elimu wa Wilaya Bi. Anna Shitindi  alieleza kwamba hali mbaya ya ufaulu kwa watoto wa shule za msingi na sekondari kwa  miaka mitatu mfululizo imekuwa ni changamoto kubwa katika Wilaya ya Kibiti kutokana na ufaulu wa wanafunzi  kushuka hali ambayo  inachangiwa na watoto kushinda na njaa wawapo shuleni, licha ya Jamii yenyewe kuwa chanzo kikubwa cha tatizo hili .

Hayo yamebainishwa katika siku ya wadau wa maendeleo ya elimu Wilaya ya kibiti ambapo Kaimu Mkuu wa Wilaya Meja Edward Gowele amewataka wadau wa Elimu kuamua kwa vitendo kufanya mapinduzi makubwa  ya elimu Wilayani humo.

“sasa ni wakati wa kuamua Kwa nguvu zetu zote kufanya mapinduzi makubwa kwenye Elimu, Elimu ni gharama na hatuwezi kukwepa, Serikali imebeba mzigo wote wa ada mashuleni wanafunzi wanasoma bure, hivyo gharama za chakula lazma sisi tuzibebe”alisema Gowele.

Katika kikao hicho Gowele aliongoza majadiliano ya wadau na kuafikiana maazimio mbalimbali baadhi ya hayo ni :- Suala la uchangiaji chakula mashuleni kuwa endelevu, kuchangia vitendea kazi shuleni, wakati huo huo wamewataka wazazi na Jamii kwa ujumla kuanzisha mashamba ya mazao ya chakula ikiwa ni pamoja na kuanzisha kambi za wanafunzi kwa madarasa ya mitihani.

Vilevile Madiwani wametakiwa kuwa desturi ya kuitisha mikutano ya Wazazi kwenye kata zao, kutoa motisha Kwa Walimu waliofanya vizuri, kujenga mifumo ya nidhamu kwa Walimu sambamba na kushawishi Vyama vya msingi kuwa na azimio la kuchangia kwenye Elimu. Hata hivyo wameazimia kutoa taarifa za takwimu za Wazazi wasiopeleka watoto Shule Ili wachukuliwe hatua, kutoa mafunzo Kwa Walimu  kazini huku wakisisitiza Viongozi wa Wilaya kutembelea kata zote na kufanya uhamasishaji kwa wazazi kuhusu masuala ya Elimu na umuhimu wake.

Vilevile mkurugenzi mtendaji wa Wilaya Mohamed Mavura licha yakuzungumzia hali mbaya ya ufaulu amewaagiza Walimu ambao shule zao zina maeneo makubwa kuhakikisha wanalima mazao ya chakula mboga na matunda Ili kuweza kufanikisha upatikanaji wa chakula kilicho bora shuleni.

“sitaki kusikia wala kuona shule hazizalishi chakula wakati kuna ardhi ya kuweza kulima mazao ya chakula” alisema Mavura.

 

Matangazo

  • KUANZA KWA MFUMO MPYA WA UKUSANYAJI MAPATO (TAUSI) March 01, 2023
  • KUANZA KWA MFUMO MPYA WA UKUSANYAJI MAPATO (TAUSI) March 01, 2023
  • TANGAZO KWA WAFUGAJI WOTE WILAYA YA KIBITI December 29, 2022
  • TANGAZO KWA WAKULIMA WOTE WILAYA YA KIBITI December 30, 2022
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • WILAYA YA KIBITI YASHEHEREKEA MIAKA 106 YA SKAUTI NCHINI

    March 11, 2023
  • UKAGUZI WA UJENZI WA VYUMBA VITANO VYA MADARASA PAMOJA NA OFISI SAMBAMBA NA UKAGUZI WA KPI (KEY PERFORMANCE INDICATORS) SHULE YA MSINGI KIASI.

    March 09, 2023
  • SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAFANA WILAYANI KIBITI.

    March 07, 2023
  • MAAFISA UGANI NA WATENDAJI WA KATA WAKABIDHIWA PIKIPIKI-WIAYANI KIBITI.

    March 06, 2023
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.