• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WAFUGAJI WILAYA YA KIBITI WATEUA VIONGOZI WA MUDA.

Posted on: August 23rd, 2023


MUSA KALAGE , ZANZIBAR MASHOA WAIBUKA KIDEDEA.

23.8.2023.

Chama cha wa wafugaji Mkoa wa Pwani kimeteua na kutambulisha Viongozi wa muda wa  wafugaji Wilaya ya Kibiti wakati wakisubiri kufanya uchaguzi Mkuu wa kikatiba, unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Zoezi hilo limefanyika Leo tarehe 23.8.2023 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo Musa Kalage ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa muda wa wafugaji Wilaya ya Kibiti huku Zanzibar Mashoa akiteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti.

" Viongozi hawa tuliowatewa leo wataongoza nafasi hizi mpaka muda wa uchaguzi wa kikatiba utakapofika ".

Akitaja sifa za kupata uongozi katika Chama Cha wafugaji, Mwenyekiti wa wafugaji Mkoa wa Pwani Ngobere Msamau amesema ili mtu ateuliwe au kuchaguliwa lazima ajue kusoma na kuandika, awe na moyo wa kujitolea, awe kiunganishi kati ya Chama Cha wafugaji na Serikali, kiunganishi wa Wafugaji na wakulima.

Vilevile Ngobere  amewataka wafugaji kuanza kubadilika kutoka katika ufugaji wa mazoea  kwenda ufugaji wa kisasa huku akiwaelekeza Viongozi walioteuliwa kuendelea na zoezi la utoaji wa elimu kwa wafugaji  ili waweze kuendana na mabadiliko kila upande utambue umuhimu wa mwenzake na Mali zake.

" Muyapokee mabadiliko, msifuge kwa mazoea, tuna zoezi la uanzishwaji wa ranchi Wataalam wanaendelea kuliratibu katika baadhi ya vijiji vyenu, lipokeeni tukafuge kisasa zaidi tuachane na maisha ya kuhamahama" .

Hata hivyo Ngobere amezungumzia suala la minada ya mifugo kutofanya kazi na kusema kwamba, uelewa wa pamoja unahitajika ili kupata /kuona namna bora ya kuifungua minada hiyo na kuanza kufanya kazi kwa kushirikiana na wafanyabiashara.

" Hii haikubaliki, mtu afugie kibiti, halafu akauzie chalinze, haikubaliki" Alisema Ngobere.

Aidha Chama cha wafugaji kimetoa zawadi ya vyeti vya utambuzi kwa baadhi ya wafugaji ambao wanasimamia amani, hawajihusishi na migogoro katika vijiji wanavyofugia .

Wafugaji waliopewa zawadi ya cheti utambuzi  ni Susa Lago, Yohana Mollel, Mkala Bujiku Ndaki,  Kisinza Imel na Daktari wa mifugo Mkoa wa Pwani ( RVO) Ramadhan Mwaiganju kwa kazi nzuri aliyoifanya ya uhamasishaji wa uanzishwaji wa ranchi  ndogondogo za kufugia mifugo ulioanza kutekelezwa katika Wilaya ya Kibiti.

Akikabidhi uongozi huo uliodumu kwa muda mrefu tangu mwaka 2009 mmoja wa wasisi wa Chama Cha wafugaji aliyekuwa Mwenyekiti wa wafugaji Wilaya ya Kibiti na Rufiji Bw. Deusi Ndaki amesema ni wakati wa kupisha na wengine kuongoza Chama yeye anapumzika.

"nimedumu kwa muda mrefu nikiwa kiongozi tangu kuanzishwa kwa Chama hiki, nachukua nafasi hii kujihudhulu kupisha wengine nao wachaguliwe kuongoza chama.

Nao baadhi ya wafugaji waliohudhuria kikao hicho, wameomba kuimarishiwa minada kwani changamoto kubwa inayowakabili ni kukosekana kwa masoko kwani wao wanaamini katika chama chao Usimamizi ukiwa imara kila kitu kitakwenda sawa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amewapongeza wafugaji kwa kuteuwa Viongozi wa muda wakati wakisubiri uchaguzi huku akiamini kuwa wanakwenda kuwa kiunganishi kizuri kati ya wafugaji, wakulima na Serikali.

"Kumekuwa na  malalamiko mengi yanayowakabili wafugaji, na haya yanatokana na kutokuwa na mfumo wa pamoja ikiwa ni pamoja na kutohudhuria vikao, badilikeni" Alisema Kanali Kolombo.

" Ili kumaliza migogoro ya wafugaji na wakulima Serikali imekuja na mpango wa uanzishwaji wa Ranchi ndogondogo, na zoezi hili linaendelea kwa sasa katika Kata ya Mtunda kwa sasa baada na kuanza na Kata ya mjawa hatutaki kusikia migogoro lipokeeni".Alisema Kanali Kolombo.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Bw.Hemed Magaro akasema ngazi ya Wilaya imejipanga kuweka mikakati ya kukuza masoko  ya mifugo na malisho ndani ya Wilaya. Pia  amewasisisitiza wafugaji kushirikiana kikamilifu kuhakikisha minada ya mifugo iliyopo Wilaya ya Kibiti inafanya kazi na kuongeza mapato ya Halmashauri yanayopotea mara kwa mara.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.