• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WANAJAMII KIBITI WAPEWA UWEZO WA KUFANYA DORIA KWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA KISASA.

Posted on: March 22nd, 2024

21.3.2024

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amefungua mafunzo muhimu ya wanajamii wa vijiji 19 vilivyopo karibu na hifadhi ya delta ya mto Rufiji yenye lengo la kuwajengea uwezo  na kushirikiana na Serikali kuhifadhi mikoko kwa njia ya Matumizi ya Mtandao wa  Kijiografia ujulikanao kama Global Mangrove Watch(GMW).

Akifungua mafunzo hayo Kanali Kolombo amewaagiza Wanajamii hao kusikiliza na kuelewa vizuri watakayofundishwa ili baada ya mafunzo wakaweze kufanya kazi kwa vitendo na weledi mkubwa.

"Nendeni mkatumie vyema mtakachopewa kupitia mafunzo haya kwa vitendo ili mkaimarishe ulinzi na Matumizi endelevu ya Mikoko iliyoko karibu na Vijiji vyenu" Alisema Kanali Kolombo.


Vilevile Kanali Kolombo amewapongeza wakazi wa Delta kwa namna wanavyoishi kwani pamoja idadi ya watu kuongezeka na kupelekea  mahitaji ya Wanajamii kuongezeka pia lakini bado Rasilimali za Mikoko zimeendelea kuwepo na kuhifadhiwa.

Mafunzo hayo yamefanyika kwa nadharia jana 21.3.2024 katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Wilaya ya Kibiti yakiendeshwa na Mkufunzi  Afisa Tehama Ndg. Kuto Edmund kutoka Ofisi ya Kanda ya Afrika Mashariki ya Shirika la Wetland International la Mjini Nairobi.

Hata hivyo mbele  ya Mkuu wa Wilaya, Mhifadhi Mkuu Frank Sima kutoka TFS Makao Makuu alifafanua kuwa  Wanajamii hao watapewa  vishikwambi ambavyo vitasaidia upashanaji wa Habari baina ya TFS na Wanajamii kama inavyoelekezwa kwenye Sheria ya Misitu namba 14 ya mwaka 2002 kifungu cha 99 ambayo inaeleza kuwa, taarifa zitakazotolewa zitakuwa sahihi kwa kuwa zinaonekana kwa njia ya Mfumo wa Kijiografia.

Naye  Mhifadhi Mkuu wa Misitu wa Wilaya ya Kibiti Ndg, Davis Mlowe alisema kuwa TFS inaendelea na itaendelea kushirikiana na Serikali za vijiji kupitia Kamati za Maliasili za vijiji vyote ndani ya Wilaya hususani katika upande wa Misitu ya Mikoko na Misitu ya Nchi kavu pia.


Aidha, Afisa Mradi wa Shirika la Uhifadhi Ardhi-oevu Ulimwenguni Upande wa Tanzania Frank Napoleon katika mafunzo hayo,  amekabidhi  vishikwambi 11 kwa Wanajamii hao ambao ni Wenyeviti na Makatibu wa Kamati za Maliasili za vijiji 19 vilivyoko karibu na Hifadhi ya Mikoko.

Mara baada ya kukabidhi  vishikwambi hivyo Afisa mradi Ndg. Napoleon alisema vifaa hivyo ni sehemu ya Utekelezaji wa randama ya Ushirikiano baina ya TFS na Shirika hilo ambapo tarehe 11.3.2024 walikabidhi ndege 2 zisizokuwa na rubani (drones)  na kishikwambi kimoja kwa TFS.


Shirika la Uhifadhi Ardhi-Oevu Ulimwenguni (Wetlands International) linatekeleza miradi mbalimbali inayoendelea kwenye mikoko nchini Tanzania, Kenya pamoja  Ethiopia kupitia Mradi ujulikanao kama "Source to Sea".


Mara baada ya kupatiwa mafunzo, Wenyeviti  na Makatibu wa Kamati za Maliasili za vijiji  wamesema kupitia mafunzo hayo wataongeza weledi wa utendaji kazi  na kupata taarifa zilizo sahihi kwa wakati. Vilevile Wanasemina hao, wamelipongeza shirika la Wetland International kwa kuandaa mafunzo na kutoa vishkwambi huku wakisema vitawasaidia kupata taarifa nyingi zaidi kwa muda mfupi zikiwa sahihi.


Mafunzo hayo yametamatishwa kwa kufanya mazoezi kwa vitendo katika Kijiji cha Nyamisati ambapo simu janja hizo (vishkwambi) ziliunganishwa na Mfumo kuweza kutambua baadhi ya maeneo yenye uharibifu ndani ya msitu wa mikoko.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.