• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WANAJAMII WA MKOA WA PWANI WANOLEWA KUWA WAKUFUNZI WA UFUGAJI NYUKI WENYE TIJA.

Posted on: November 1st, 2024

Wanajamii wa Wilaya za Kibiti, Mkuranga Kisarawe, Rufiji na Bagamoyo Mkoa wa Pwani kwa uwakilishi wa vikundi vyao wamepatiwa mafunzo ya siku 2 ya ufugaji wa nyuki yaliyofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Halmashauri ya Kibiti ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuhifadhi Mazingira.


Mafunzo yamelenga kutoa uelewa wa pamoja juu ya mazao ya nyuki, kuwaandaa Wanavikundi vya ufugaji nyuki kuwa wahifadhi wakuu wa mazingira katika maeneo yao. Pia yamelenga kuelimisha namna bora ya kuzalisha mazao mengi na safi ya nyuki kwa kutumia rasilimali ya misitu iliyopo vijijini sambamba na kujipatia ajira ambayo itawawezesha kupata kipato na kujikimu kiuchumi.


Washiriki hao wamefundishwa kutambua namna na sababu ya kuanza ufugaji, mazao ya nyuki, manaeneo yanayostahili kuweka mizinga (manzuki) aina ya nyuki, faida za mazao ya nyuki n.k.

 Licha ya kupewa uelewa wa pamoja washiriki hao wamefanya mafunzo kwa vitendo ambapo wamefundishwa kutambua maadui wanaofukuza nyuki kwenye mizinga na namna ya kuidhibiti, kutengeneza vianzio vya masega, namna ya kutundika mizinga na namna ya kutumia vifaa mbalimbali vya nyuki kama vile mavazi ya kujikinga, mashine ya kukamua na kupakia asali

Washiriki hao wamesema wamefarijika sana kupata  mafunzo kwani  yamewapatia uelewa wa pamoja kwa kubadilishana mawazo na kutengeneza uwanda mkubwa zaidi wa ufugaji nyuki. Vilevile wamesema wanatarajia vikundi vilivyopo kuanza kufanya kazi baada ya kujua namna ya kutumia mizinga huku wakihamasishana kuungana kwa pamoja kuweza kuwa na ufugaji nyuki wenye tija Mkoa wa Pwani.


Awali Mtathimini na Mfuatiliani wa shughuli za mradi huo Bi. Donata Didas aliwataka washiriki wote kuwa wasikivu kwani mafunzo hayo yatawajengea uelewa wa pamoja, huku akitarajia kuwa wanakwenda kuwa mabalozi wazuri kwa kutoa elimu katika maeneo wanayotoka wakiwa wakufunzi Wakuu.


Aidha, Mratibu wa mradi huo Wilaya ya Kibiti Ndg, Dotto Mandago  amesema mafunzo hayo yatasaidia kukuza tasnia ya ufugaji nyuki kuwa endelevu na tayari kwa Kibiti wamekwishapokea mizinga 10 ya kuanzia kazi. Pia amewasitiza washiriki wote kwenda kuwa walimu wazuri kwa wanajamii ambao hawakupata bahati ya kushiriki.

TaTEDO-SESO ni  Taasisi ya kiraia ya inayoendeleza huduma ya nishati endelevu yenye lengo la kuboresha maisha ya jamii kwa kuongeza upatikanaji wa huduma za nishati endelevu kwa  kupitia mradi Jumuishi wa kuhifadhi Misitu na kuboresha mnyororo wa thamani wa mkaa unaofadhiliwa na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya waliowezesha mafunzo hayo kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania chini ya Wizara ya Fedha


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.