• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WILAYA YA KIBITI YASHEHEREKEA MIAKA 106 YA SKAUTI NCHINI

Posted on: March 11th, 2023

11/3/2023.

Chama cha skauti Wilayani Kibiti kimeadhimisha miaka 106 ya kuanzishwa kwa skauti Tanzania bara, katika viunga vya shule ya Sekondari Zimbwini na kuhudhuriwa na makundi ya  wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi na Sekondari.

Skauti Tanzania ilianzishwa tarehe 22/2/1917(Tanganyika) ikitokea Zanzibar ambako ilianzishwa mwaka 1912.

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya kaimu Katibu tawala Bw. Lucas Magai amesema, ili kukuza vijana wenye maadili watakao iendeleza nchi baadaye, kuna kila sababu ya kuwa na mafunzo ya skauti katika shule zote ndani ya wilaya hususani vijana wanaoishi maeneo delta.

“Mkawe na mafunzo ya skauti katika shule zote Wilaya ya Kibiti, yatakayosaidia kulea vijana katika maadili mema, uzalendo na kujitegemea ili kujenga Taifa imara.” Alisema Magai.

Magai aliendelea kusema kuwa, uwepo wa makundi ya skauti yanayopata mafunzo na kuyaishi kama skauti ilivyokusudia ni muhimu sana katika ulimwengu wa leo kwani ni dhahiri kuwa tutatengeneza vijana waadilifu wanaojua wajibu wao kwa Mungu, Nchi na wao binafsi kama ilivyo katika kiapo cha skauti nchini.

Vilevile kutokana na changamoto zilizobainishwa katika risala ya wanafunzi na Kamishna wa skauti, Magai amesema amezipokea na atazifikisha mahala husika ili ziweze kutatuliwa huku akiwataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao, kwani elimu ni ufunguo wa Maisha yao .

Aidha Kamishna wa skauti wilaya ya Kibiti ndg. Dotto Mandago amesema, lengo la kuanzishwa kwa skauti duniani na nchini kwetu ni kuwafundisha vijana uzalendo, kuipenda nchi yao kuwafundisha vijana stadi za kazi za maisha ya kujitegemea, kuwaheshimu Viongozi wao na kuja kuwa Viongozi bora baadaye. Pia Kamishna Dotto aliendelea kusema kuwa, skauti hufundisha vijana namna ya kuona umuhimu wa kuilinda nchi yao, kutunza rasilimali zilizopo na kuwafanya vijana kuwa wakakamavu ambapo watakuwa tayari kutetea maslahi ya umma muda wowote.

Akisoma risala kwa niaba ya wanafunzi Shakira Sume amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana kupitia chama cha skauti nchini, katika ngazi ya Wilaya wanakabiliwa na changamoto ya uelewa mdogo wa jamii kuhusu kuitambua skauti, kutopata mafunzo ya uokoaji, ukosefu wa ofisi rasmi ya Kamishna, ukosefu wa vifaa vya michezo mbalimbali, ukosefu wa maeneo ya kufanyia miradi mashuleni na baadhi ya wazazi kushindwa kumudu gharama za Kambi Kwa watoto wao.

Aidha katika risala hiyo wanafunzi wamemwomba mlezi  wa skauti, kuwasaidia kujenga ofisi ya kamishna wa skauti  wilayani, wameomba kutafutiwa wataalamu wa skauti Kwa ajili ya kuwajengea uwezo n.k.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.