• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

ZILIZOKUWA KAMBI ZA MAFURIKO KIBITI ZAVUNJWA RASMI.

Posted on: June 24th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo akiwa ameambatana na Kamati ya maafa pamoja na Viongozi wa Chama amezivunja rasmi kambi zilizotengwa kwaajili ya waathirika wa mafuriko Wilayani humo. Kanali Kolombo ametekeleza jukumu hilo katika kambi ya kitumbini tarehe 21.06.2024. Kambi hiyo iliyokuwa katika Kata ya Mtunda ilikuwa ni hifadhi kuu ya waathirika wa mafuriko Wilayani Kibiti.

Uamuzi huo wa kuvunja kambi umefikiwa baada ya mvua kuisha na maeneo yaliyoathirika kuonekana kurejea katika hali yake ya kawaida.

Akifunga kambi hiyo Kanali Kolombo amewaeleza wananchi kuwa  ngazi ya Wilaya imekwishapata mbegu za muda mfupi hivyo wanaporejea katika makazi yao wakalime na kupanda mbegu hizo ili waweze kujiandalia chakula cha baadaye.

"Mliomba mbegu, tumekwishazipata, mtagawiwa katika Vitongoji mnavyotoka orodha yenu tunayo, mkapande mbegu hizo" Alisema Kolombo.

Mbali na upatikanaji wa mbegu amewaondoa hofu wananchi hao kwa kuwahakikishia kuendelea kuishi salama waendako kama walivyokuwa wameimarishiwa ulinzi kambini hapo.

Vilevile Kanali Kolombo ametoa shukrani zake za dhati kwa Mhe. Rais SSH kwa misaada aliyotoa, wadau mbalimbali, viongozi wa ndani na nje ya Wilaya kwa namna walivyojitoa kuhakikisha familia hizo zinakuwa salama.

Kuhusu maombi ya wananchi hao kupata makazi ya kudumu Mratibu wa Kamati ya maafa Wilaya ya Kibiti Ndg. Zakayo Gideon ametoa rai kwa wananchi kuridhia kwenda katika maeneo watakayogawiwa  kwani mpaka sasa wamekwishapata maeneo katika Kata ya mahege ambayo ni Tomoni na Nyakinyo wakati wakisubiri maeneo mengine.

Hata hivyo katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kibiti Ndg. Maliki Magimba akitoa Salamu za Mwenyekiti wa Chama na Mhe. Mbunge amewataka wananchi hao kushukuru Mungu kwa kila jambo na kuganga yajayo. Badala ya kukumbuka yaliyopita basi wachangamkie kilimo kwani tayari mbegu zimewasili.

Nao Wananchi waliopata hifadhi kambini hapo wameishukuru Serikali na Uongozi wote kwa namna walivyowapokea na kuwahudumia kwa kila hali ikiwemo kuimarishiwa ulinzi.

Aidha kabla ya kuondoka Kambini hapo wameiomba Serikali kuendelea kuwaimarishia ulinzi hususani katika mashamba yao kutokana na changamoto ya Mifugo, waliomba kupewa maeneo ya makazi ya kudumu na kuhakikisha mbegu hizo zinagawiwa katika Vitongoji vyote.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.