• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

APATIKANA AKIWA AMEFARIKI BAADA YA KUPOTEA KWA MUDA WA WIKI MOJA

Posted on: November 18th, 2022

Mtoto wa miaka  kumi na mbili ( 12) Mkazi wa kibiti kusini aliyejulikana  kwa jina la Ibrahim Mohamed Kakatu, mwanafunzi wa darasa la 6 katika shule ya msingi Kibiti amepatikana akiwa amefariki katika eneo  la Mtawanya A kitongoji cha Umikendo  Kata ya Mtawanya Wilaya ya Kibiti baada ya kupotea tangia tarehe 12 mwezi Novemba mwaka huu akiwa anacheza na wenzake.

Jeshi la Polisi Wilaya ya  Kibiti lilifika eneo  la tukio ambapo mwili wa marehemu umepatikana katika  Kijiji cha Mtawanya A,  baada ya taarifa kutolewa na msamaria mwema aliyeuona mwili huo jina limehifadhiwa kwa usalama zaidi  na uchunguzi unaendelea.

Kwa mujibu wa Daktari Mashauri Matiku wa kituo cha afya cha Kibiti ambaye alifika eneo  la tukio kufanya  uchunguzi wa kitaalam kutambua chanzo cha kifo hicho amesema ni vigumu kutambua kwani mwili ulikwisha haribika.

Kwa mujibu wa taarifa za awali mpaka siku marehemu Ibrahimu anapotea alikua akicheza na wenzake ndipo akatokea mtu asiyejulikana na kuuliza kati yao ni nani anaejua kuendesha baiskeli? Ndipo marehemu alijibu kuwa anajua hivyo mtu huyo akampa sh. 3000 na kumwagiza kwenda kumkodishia baiskeli matokeo yake Ibrahimu hakurudi  mpaka mwili wake kupatikana akiwa amefariki.

Aidha, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Meja Edward Gowele akiambatana na viongozi wa ulinzi na usalama wameshiriki katika zoezi la kuhifadhi mwili wa marehemu Ibrahimu na akiwa  hapo Mhe. Gowele amesikitishwa nakulaani vikali mauaji  ya  kijana huyo, vilevile ameagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuchunguza na kuhakikisha  waliohusika na mauaji  wanapatikana na kuchukuliwa hatua za kisheria. Vilevile ameagiza nakusisitiza kwa wamiliki wote wa mashamba pori waliotelekeza maeneo yao bila kulima wala kusafishwa  wahakikishe yanakuwa wazi muda wote kuanzia sasa kwa ajili ya usalama na pia amewataka wananchi kuachana na Imani potofu ikiwemo Ushirikina kwani zinachangia sana vitendo  hivyo viovu.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.